Interahamwe

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Bendera ya Interahamwe

Interahamwe ilikuwa kundi la wanamgambo lililoanzisha mauaji ya kimbari nchini Rwanda mnamo 1994. Katika mauaji hayo, takriban milioni moja ya raia, hasa Watutsi lakini pia Wahutu wasiochukiana nao, waliuawa[1][2].

Interahamwe ilianzishwa mnamo 1990 kama tawi la vijana la National Republican Movement for Democracy and Development (MRND kwa kifupi chake cha Kifaransa).

Interahamwe walifukuzwa Rwanda na jeshi la Rwandan Patriotic Front (RPF) katika vita ya wenyewe kwa wenyewe ya Julai 1994. Wametangazwa kuwa kundi la kigaidi na serikali nyingi za Afrika na kimataifa. Interahamwe na makundi yaliyotokana nayo wanaendelea kupiga vita ya msituni dhidi ya Rwanda kutoka vituo vyao katika nchi jirani.

Mbinu[hariri | hariri chanzo]

Interahamwe mara nyingi walitumia mapanga ('mupanga' kwa Kinyarwanda) kwa kutekeleza mauaji, lakini bunduki, mabomu na zana nyingine zilitumika pia.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. Reyntjens, Filip (21 October 2014). "Rwanda's Untold Story. A reply to "38 scholars, scientists, researchers, journalists and historians"". African Arguments.  Check date values in: |date= (help)
  2. Des Forges, Alison (March 1999). Leave None to Tell the Story: Genocide in Rwanda – The Organization → The Militia. New York: Human Rights Watch. ISBN 1-56432-171-1. Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2021-03-07. Iliwekwa mnamo 2020-05-31.  Check date values in: |date= (help)
Makala hii kuhusu mambo ya kihistoria bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Interahamwe kama enzi zake au matokeo yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.