Edmund Hillary

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Edmund Hillary huko Antarctica

Edmund Percival Hillary (20 Julai 1919 - 11 Januari 2008) alikuwa mpelelezi kutoka New Zealand aliyejulikana hasa kutokana na milima mingi aliyopanda.

Pamoja na sherpa Tenzing Norgay alikuwa mwanadamu wa kwanza wa kufika kwenye kilele cha Mlima Everest tarehe 29 Mei 1953.

Alijifunza kupanda milima tangu utoto wake kwao New Zealand. Alifanya kazi ya kufuga nyuki iliyomwezesha kutumia miezi ya majira ya baridi ya New Zealand kwa safari zake duniani.

Hillari alikuwa pia mtu wa kwanza aliyevuka bara la Antaktika kwa trekta.

Makala hii kuhusu mtu huyo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Edmund Hillary kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.