Angata Barrikoi

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mtaa mdogo wa Angata Barrikoi.

Angata Barrikoi ni kata inayopatikana katika kaunti ya Narok, Kenya.

Eneo ni la km² 315.20.

Watu[hariri | hariri chanzo]

Ina watu wanaokadiriwa 24,945 (2019) na vijiji vidogo kama: Kabusa, Oldonyorok, Ongata, Tebengwet, Kabchinese, Kabwolta, Kondamet, Leoboinet na Sacfo.

Makabila[hariri | hariri chanzo]

Kuna makabila mengi kama Wakikuyu, Wakisii lakini Wakipsigis ni 10,000. Kuna Wasomali ambao wanafanya biashara katika maduka.

Dini[hariri | hariri chanzo]

Kuhusu dini, wanakadiriwa watu elfu kumi ni Wakristo, lakini watu wengi huchanganya dini za jadi na za Kikristo, hivyo ni ngumu kutambua. Wengi ni Waprotestanti na mia tisa ni wa dini za jadi.

Hakuna msikiti.

Kilimo na ufugaji[hariri | hariri chanzo]

Watu wengi wanafuata ufugaji wa ng'ombe na pia mbuzi na kondoo. Lakini pia watu wanalima hasa mahindi na pia maharagwe. Mboga kama sukuma wiki pia inapendwa sana na kuliwa na watu wengi.

Masoko[hariri | hariri chanzo]

Kuna vijisoko vidogo kama: soko la Ongata na la Oldonyorok. Pia kuna maduka mengi na maghala ambapo nafaka kama mahindi huwekwa na kuuzwa. Pesa zinazotumika ni Shilingi ya Kenya na Shilingi ya Tanzania.

Masomo[hariri | hariri chanzo]

Shule nyingi zimejengwa ili wanafunzi wasome[1], kama shule za sekondari za Ongata[2] na 0ldonyorok. Pia kuna vyuo vingi, hasa cha Oldonyorok, ambapo mambo ya ufundi hufundishwa.

Basi la shule ya Angata Barrikoi.

Afya[hariri | hariri chanzo]

Vituo vya matibabu ni vichache mno, kituo kinachojulikana ni Angata Health Centre[3][4]. Kuna famasia nyingi hasa katika maduka ya Angata na Oldonyorok.

Michezo[hariri | hariri chanzo]

Kuna timu ya mpira wa miguu inayoitwa Angata Victors FC.

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]