Xscape

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Xscape
ChimbukoAtlanta, Georgia, U.S.
Miaka ya kazi1991–2001; 2005–2009
StudioSo So Def/Columbia/SME Records (1992-1998)
Ameshirikiana naBow Wow, Jermaine Dupri
LaTocha Scott
Tamika Scott
Tameka "Tiny" Cottle
Kandi Burruss
Kiesha Miles
Tamera Coggins-Wynn

Xscape lilikuwa kundi la waimbaji wa kike wa R&B kutoka Atlanta, Georgia nchini Marekani. Kundi lilipata platinamu tatu mfululizo kwa albamu zao ikiwa ni pamoja na kushika nafasi ya 6 na kuingiza vibao 10 bab-kubwa katika chati za Billboard Hot 100 katika kipindi cha miaka ya 1990 - "Just Kickin' It", "Who Can I Run To", "The Arms of the One Who Loves You", na "My Little Secret". Kikosi halisi cha kundi kiliunganishwa na ndugu ambao ni LaTocha na Tamika Scott, Kandi Burruss, Tameka "Tiny" Cottle, na Tamera Coggins, lakini Coggins aliondoka kabla kundi halijatoa hata albamu yao ya kwanza.

Historia[hariri | hariri chanzo]

LaTocha na baba wa Tamika Scott, Rev. Randolf Scott, walikuwa sehemu ya kundi la R&B Scott Three mwanzoni mwa miaka ya 1970. Ndugu hawa walifundishwa kuimba na baba yao wkaiwa katika umri mdogo kabisa. Wanaimba kanisani na baadaye wanaenda kwenye mashindano ya watoto wenye vipaji huku wakikua. Mwanzoni mwa miaka ya 1990, wakakutana na wanachama wengine watatu wa Xscape, Kandi Burruss, Tamera Coggins-Wynn, na Tameka "Tiny" Cottle katika tumbuizo la kisanaa la shulel, Tri-Cities, huko mjini East Point, Georgia, nje kidogo ya mjini wa Atlanta. Baba wa Cottle, Charles Pope, na mjomba'ke, Joseph Pope (1933–1996), walikuwa wanachama wa kundi la R&B, The Tams.

Diskografia[hariri | hariri chanzo]

Studio albamu[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya Nje[hariri | hariri chanzo]