Windows XP

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Windows XP ni toleo la mfumo wa kazi wa tarakilishi uliokuwa miongoni mwa Windows zenye kufanya kazi kwa ufanisi zaidi kuliko zile za zamani, kama Windows 95, Windows 98 na Windows Millenium.

Sifa za Windows XP[hariri | hariri chanzo]

  1. Wepesi wa kuanza na kumaliza kutumia.
  2. Uwezo wa kutumia lugha mbili, kwa mfano Kiingereza na Kiarabu, pia uwezo wa kubadilisha lugha hizo na kuweka nyengine.
  3. Kufungua kurasa kwa haraka.
  4. Uwezo wa kuendesha programu zaidi ya moja kwa wakati mmoja.
  5. Uwezo wa kuhifadhi vitufe (files) vilivyofutwa katika kapu (recycle bin).
  6. Uwezo wa kufanya kazi katika mdahalishi (network) kwa haraka.
  7. Uwezo wa kubadilishana vitu (data) kati ya programu tofauti.
  8. Kutumia majina marefu (zaidi ya herufi 255 katika jina la faili moja).
  9. Haraka na wepesi katika utekelezaji.
  10. Vifaa vya kisasa vinavyowezesha kufanya kazi katika net.
  11. Uwezo wa kutambua idadi nyingi za vyombo vilivyounganishwa ndani ya kumpyuta.
  12. Uwepo wa picha nyingi zenye kuvutia kwa ajili ya kupamba skirini (Backgrounds).

Kuanza kutumia Windows[hariri | hariri chanzo]

Kabla hujaanza kutumia Windows unatakiwa kufanya mambo yafuatayo:

  • 1. Kuhakikisha waya wa umeme umeshaunganishwa kwenye kompyuta yako.
  • 2. Kufungua kompyuta kwa kutumia sehemu inayoitwa power.
  • 3. Kusubiri mpaka idhihiri sehemu inayoitwa desktop.