Wilaya ya Kalambo
Wilaya ya Kalambo | |
Location in Tanzania |
|
Majiranukta: 8°18′12″S 31°31′10″E / 8.30333°S 31.51944°E | |
Country | Tanzania |
---|---|
Region | Rukwa Region |
Kalambo ni jina la wilaya mpya katika mkoa wa Rukwa yenye postikodi namba 55400[1], ambayo ilianzishwa rasmi mnamo Machi 2012.[2]
Makao makuu ya wilaya yako Matai.
Mkuu wa wilaya wa kwanza alikuwa Moshi Chang'a. [3]
Wilaya limepokea jina kutoka mto Kalambo unaopita hapa hadi kuishia kweye Maporomoko ya Kalambo upande wa Zambia.
Idadi ya wakazi wa wilaya ilikuwa 207,700 wakati wa sensa ya mwaka 2012. [4]
Uchumi[hariri | hariri chanzo]
Eneo la Kalambo liko kati ya Sumbawanga mjini na mpaka wa Zambia. Barabara ni chache na mbaya. Wakazi wengi hulima na kufuga. Mazao ya sokoni ni pamoja na mahindi, alizeti, maharagwa, muhogo na asali.[3] Watu wachache wanalima madini na kuvua samaki.[3]
Utawala[hariri | hariri chanzo]
Katika uchaguzi wa bunge la Tanzania Kalambo ni jimbo la uchguzi.[5]
Kata[hariri | hariri chanzo]
Wilaya ya Kalambo huwa na kata 17:[6]
|
|
Marejeo[hariri | hariri chanzo]
- ↑ https://www.tcra.go.tz/images/documents/postcode/rukwa.pdf[dead link]
- ↑ Staff. "Tanzania: State Gazettes New Regions, Districts", 9 March 2012. Retrieved on 2014-01-13. Archived from the original on 2012-08-23.
- ↑ 3.0 3.1 3.2 Siyame, Peti. "Tanzania: Truance Irks Kalambo DC", 3 July 2012.
- ↑ Sensa ya 2012, Rukwa - Kalambo District Council
- ↑ Organisations located in Rukwa Region - Tanzania. African Development Information. Jalada kutoka ya awali juu ya 2018-06-01. Iliwekwa mnamo 2014-01-13.
- ↑ Postcodes Rukwa Region 55000. Tanzania Communications Regulatory Authority (TCRA) (2012). Jalada kutoka ya awali juu ya 2012-08-31. Iliwekwa mnamo 2014-01-13.
![]() |
Kata za Wilaya ya Kalambo - Mkoa wa Rukwa - Tanzania | ![]() |
---|---|---|
Kasanga | Katazi | Katete | Kilesha | Kisumba | Legeza Mwendo | Mambwekenya | Matai | Mkali | Mkowe | Mnamba | Msanzi | Mwazye | Mwembenkoswe | Mwimbi | Sopa | Ulumi |