Wikipedia:Jamii

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

English | Kiswahili | Francais | Deutsch (+/-)

Uhamasishaji/Utangazaji[hariri chanzo]

Malengo:

  • Kutengeneza kamusi elezo kubwa ya Kiswahili itakayotumiwa na mtu yeyote bila gharama
  • Kutafuta matumizi ya kamusi elezo hii mashuleni na kwenye miradi mbalimbali ya kielimu; kutumia yaliyomo ndani ya kamusi elezo hii (ambayo inapatikana kwa lugha mbalimbali)kwa faida za wazungumzaji wa Kiswahili na wale wanaojifunza Kiswahili
  • Kushirikiana na wanafunzi wa vyuo vikuu na walimu wa lugha kuchangia na kuendeleza matumizi na mchango wa kazi hii

Kinachotakiwa:

Watu wenye nia ya kushiriki[hariri chanzo]

  • Sultanseifu (Tanzania)
  • Ndesanjo
  • Sj (Boston)
  • Jeff (Toronto)
  • Mshairi (Uingereza)
  • Richard Mabala (Ethiopia/Tanzania)
  • Joseph Tungaraza(Oz)
  • Makene (Texas)
  • Stan
  • Herry Ibrahim (Tanzania) (Revolución) kutoka Florida
  • maitha (kenya)
  • Zablon Mgonja(Mtanzania) Chuo kikuu cha FISK marekani
  • Matt Crypto (UK)

Walimu na wanafunzi

Chuo Kikuu cha Nairobi
Chuo Kikuu cha Dar-es-Salaam
Shule za sekondari
Kwingineko wanakofundisha lugha

Wanablogu wa Kiswahili na wataalamu wa teknolojia ya kompyuta

Wanablogu wa Kenya naTanzania
Uhamasishaji wa mdomo kupitia watu mbalimbali kama Ory, Ndesanjo, Jeff, Joseph, Nkya, Maitha, n.k.

Mambo ya awali ya kuweka kwenye kamusi elezo[hariri chanzo]

Orodha ndefu: makala fupi za msingi za maarifa duniani; tuanze na makala 1000.

Makala zilizoko kwenye kamusi elezo za Kiingereza, Kifaransa, Kijerumani, n.k. zinaweza kusaidia wanaoshiriki kuandika makala za awali za Kiswahili

Orodha fupi:


Mapendekezo ya mambo mengine ya kujumuisha katika kamusi elezo hii yanakaribishwa.

Mikutano ijayo[hariri chanzo]

Kawaida mikutano hufanyika kupitia teknolojia ya IRC

Mkutano wa mwisho ulipangwa kufanyika jumamosi ya tarehe kwanza, Oktoba, 2005.


Malengo ya kutimiza kabla ya mkutano ujao:

#1: kuongeza idadi ya washiriki katika mkutano ujao
#2: kuongeza idadi ya watu watakaoshiriki kuhariri kamusi elezo hii
#3: kutafsriri ukurasa wa wikipedia:jamii 
#4: kuweka viunganishi vya makala au mambo yanayohusiana ndani ya makala mbalimbali za Kiswahili

Tafadhali weka maoni na mawazo yako katika ukurasa wa mazungumzo. Sj