Nenda kwa yaliyomo

Watrapisti

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Abasia ya Citeaux.

Watrapisti (ufupisho wa jina la shirika lao ni OCSO, Ordo Cistercensium Strictae Observantiae) ni wamonaki wa Kanisa Katoliki wanaofuata kikamilifu urekebisho wa umonaki wa Kibenedikto ambao ulianza Citeaux (leo nchini Ufaransa) tarehe 21 Machi 1098 ukaenea haraka kila mahali katika karne ya 12, hasa kutokana na mvuto wa mwanashirika Bernardo wa Clairvaux.

Jina linatokana na monasteri ya La Trappe, Normandy, ambapo mwaka 1664 Armand Jean le Bouthillier de Rancé alianzisha tapo lenye msimamo mkali zaidi kuhusu kazi za mikono, kimya, kujinyima chakula, kujitenga na ulimwengu na kukataa masomo mengi.

Mwishoni mwa mwaka 2020) walikuwa 1,608 (mapadri 500 hivi) kwenye monasteri 87 katika mabara yote [1].

Wasitoo wengine wote wanaunda shirikisho la O.Cist..

  1. Ordine dei Cistercensi della Stretta Osservanza (OCSO) Trappisti, katika gcatholic.org.
  • Plouvier, M. and Saint-Denis, A. (eds.), 1998: Pour une histoire monumentale de Cîteaux, 1098-1998 (Commentarii cistercienses. Studia et documenta, 8), Cîteaux.

Viungo vya nje

[hariri | hariri chanzo]
Wikimedia Commons ina media kuhusu:

Picha za Citeaux

[hariri | hariri chanzo]
Makala hii kuhusu Kanisa Katoliki bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Watrapisti kama historia yake au maelezo zaidi?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.