Sevilla

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Kanisa Kuu na ofisi ya kale ya kikoloni "Archivo de Indias"
Jumba la Alcazar lilijengwa na mafundi Waislamu kwa niaba ya wafalme wakatoliki

Sevilla ni mji mkubwa kando la mto Guadalquivir katika kusini ya Hispania na mji mkuu wa jimbo la kujitawala la Andalusia mwenye wakazi 700,000.

Historia[hariri | hariri chanzo]

Mji ulianzishwa zamani za Wafinisia ukaendelea kukaliwa na kutawaliwa na Waroma wa Kale, Wavandali halafu na Wavisigothi na tangu 711 na Waarabu Waislamu. 1248 ulivamiwa na wafalme wa Kastilia na kubaki upande wa Hispania ya kikristo.

Majengo mengi mazuri yanatunza kumbukumbu ya historia hii. Boma la Alcazar lilijengwa na mafundi waislamu kwa niaba ya wafalme wakatoliki. Sevilla ilikuwa na ofisi kuu ya utawala kwa koloni za Hispania katika Amerika.

Tovuti za Nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu maeneo ya Hispania bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Sevilla kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.