Selo

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Selo kutoka mbele na upande

Selo (Kiing. Cello, tamka chello) ni ala ya muziki inayotumia nyuzi kwa kutoa sauti. Jina lake linatokana na lugha ya Kiitalia na ni kifupi cha jina kamili violoncello[1].

Selo ni kama fidla kubwa inayosimama kwenye sakafu ikishikwa kati ya miguu ya mpigaji wake. Inapigwa kwa kutumia upinde lakini wakati mwingine pia kwa vidole[2].

Selo ni ala maarufu sana. Ina matumizi mengi: kama ala ya pekee, katika muziki wa kundi dogo na pia katika okestra. Mara kwa mara hutumiwa pia na wanamuziki wa pop, kwa mfano na Beatles.

Sehemu za selo zinafanana na zile za violini. Nyuzi zimewekwa kwa sauti za C-G-D-A, (chini hadi juu).

Selo ina sauti inayopendeza. Huanza oktava mbili chini ya C katikati, lakini inaweza kwenda juu sana. Kwa noti za juu zaidi mpigaji anaweza kutumia "nafasi ya kidole gumba" (mpiga fidla hawezi kufanya hivi). Hii ina maana kwamba kidole gumba cha kushoto kinabonyeza chini kwenye nyuzi moja au mbili juu juu ya ubao wa vidole ("juu" inamaanisha "karibu na daraja" ambapo noti za juu ziko. Kwa kweli, iko karibu na sakafu). Ingawa muziki wa selo mara nyingi huandikwa kwenye bass, muziki wa selo mara nyingi huenda juu kabisa ili kitambulisho cha sauti ya tatu kitumike haswa kama selo inapigwa peke yake.

Wapigaji selo mashuhuri ni pamoja na Yo-Yo Ma, Julian Lloyd Webber, Octavia Philharmonic, Mischa Maisky, Kirill Rodin, Tim Hugh, Robert Cohen, Ruslan Biryukov, Pieter Wispelway na Truls Mørk . Kati ya bendi za pop zinazutumia selo hasa iko Apocalyptica wanaopiga muziki wa metallica.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. Violoncello, kamusi ya Merriam-Webster, iliangaliwa Septemba 2022
  2. https://www.britannica.com/art/stringed-instrument stringed instrument, Encyclopedia Britannica online, iliangaliwa Septemba 2022
WikiMedia Commons
WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu: