Sale (mji)

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Picha ya angani ya Salé pamoja Rabat mtoni Bou Regreg; Salé iko kaskazini na Rabat kusini mto

Salé ni mji wa Moroko.

Uko ufukoni wa Atlantiki kwenye mdomo wa mto Bou Regreg ng'ambo ya Rabat mji mkuu.

Salé ilianzishwa katika karne ya 11 BK.

Mwaka 1162 Jamhuri ya Kiitalia ya Genua ilijenga hapa bandari na kituo cha kijeshi. Mji ulivamiwa na mfalme wa Wamuwahid Abd al-Mu'min. Katika karne ya 17 BK Salé ilikuwa mji mkuu wa Jamhuri ya Bou Regreg.