Jamhuri ya Bou Regreg

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Eneo la mdomo wa mto Bou Regreg
Boma la Oudaias lilikuwa makao makuu ya maharamia wa Bou Regreg

Jamhuri ya Bou Regreg (pia Jamhuri ya Sale) ilikuwa dola dogo katika eneo la miji Rabat na Sale, mdomoni mwa mto Bou Regreg, lililoanzishwa mwaka 1627.

Watawala walikuwa maharamia waliounda serikali baada ya mwisho wa utawala wa ufalme wa Wasaadi.

Halmashauri ya wawakilishi ilimteua nahodha mkuu wa jahazi za haramia na pia magavana wa Rabat na Sale.

Maharamia walishambulia hasa jahazi za nchi za Wakristo. Miji yote miwili ikatajirika. Majengo mengi ya kitovu cha kihistoria ya Rabat yalijengwa wakati ule.

Mwaka 1668 wenyeji walipaswa kukubali utawala wa wafalme Waalawi lakini hali halisi waliendelea kujitegemea hadi mwaka 1818.