Ruth Habwe

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Ruth Habwe (aliyefariki 1996) alikuwa mwanaharakati na mwanasiasa kutoka Kenya.

Maisha ya mapema na kazi[hariri | hariri chanzo]

Habwe alikuwa mwanzilishi kati ya wale wanaofanya kazi kuendeleza masuala ya wanawake nchini Kenya. Akiwa amefunzwa kama mwalimu katika Chuo cha Mafunzo ya Ualimu cha Kabete, baadaye alihudhuria Shule ya Jeanes pamoja na Margaret Koinange na Muthoni Likmani. [1] Alikuwa kiongozi wa mwanzo wa Maendeleo Ya Wanawake, ambayo aliongoza kutoka Mwaka 1968 hadi Mwaka 1971. Wakati wa uongozi wake shirika lilipitisha maazimio ya kutaka mambo kama vile kudahiliwa kwa wanawake zaidi katika kitivo cha Chuo Kikuu cha Nairobi na hali sawa za ajira. [2] Habwe aligombea ubunge mnamo mwaka 1964, akiwa mmoja wa wanawake wachache kupinga kutawaliwa kwa wanaume katika chombo hicho. Uamuzi huo haukuwa bila mabishano; [3] alishindwa kupata uungwaji mkono kutoka kwa chama chake cha kisiasa, Kenyan African National Union, na hivyo kugombea kama mtu huru. Hili liliudhi sana uongozi wa chama hadi akafukuzwa uwanachama. Swala hili lilifanya wabunge wengine "kurudi Jikoni na kuwapikia watoto wa Bw. Habwe". [4] Habwe alikuwa mtu wa kabila la Waluhya . [5] Alikuwa na watoto watano. [1] [6] [7]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. 1.0 1.1 Professor Henry Louis Gates, Jr.; Professor Emmanuel Akyeampong; Mr. Steven J. Niven (2 February 2012). Dictionary of African Biography. OUP USA. ku. 1–. ISBN 978-0-19-538207-5.  Check date values in: |date= (help)
  2. Kathleen E. Sheldon (2005). Historical Dictionary of Women in Sub-Saharan Africa. Scarecrow Press. ISBN 978-0-8108-5331-7. 
  3. Godwin R. Murunga; Shadrack W. Nasong'o (15 March 2007). Kenya: The Struggle for Democracy. Zed Books. ku. 180–. ISBN 978-1-84277-857-9.  Check date values in: |date= (help)
  4. Iris Berger (26 April 2016). Women in Twentieth-Century Africa. Cambridge University Press. ku. 100–. ISBN 978-0-521-51707-2.  Check date values in: |date= (help)
  5. Bea Sandler (1970). The African Cookbook. Carol Publishing Group. ku. 5–. ISBN 978-0-8065-1398-0. 
  6. https://www.oxfordreference.com/view/10.1093/acref/9780195382075.001.0001/acref-9780195382075-e-0784
  7. https://www.jstor.org/stable/523777