Pasta

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Aina za pasta
Aina za pasta

Pasta ni neno lenye asili ya Kiitalia kinachojumlisha chakula cha tambi kilichotengenzewa kwa kutumia unga wa nafaka (hasa ngano) na maji.

Aina ya pasta inayofahamika zaidi ni spaghetti. Lakini kuna aina nyingi za pasta.

Chanzo cha pasta hufanana kiasi na ugali yaani unga (wanga) unakorogwa na maji isipokuwa maji ni baridi. Kinyunga kinachotokea ni imara sana hukatwa kwa vipande vidogo venye maumbo mbalimbali na kupikwa kama vipande vya pekee. Kama pasta imekauka inatunzwa kwa muda mrefu hauozi na inapikwa haraka. Madukani inauzwa kama pasta kavu.

Kuna namna nyingi za kubadilisha kinyungo asilia kwa kuongeza mayai, mafuta, jibini na vingine ndani yake.

Utamu wa chakula cha pasta unakuja pamoja na mchuzi au supu zake.

Chanzo cha pasta iko katika Italia lakini zimeenea kote duniani. Ila tu hadi leo Italia ni nchi yenye aina nyingi za pasta hizi. Tambi za kufanana lakini kwa namna tofauti zinatoka katika Asia ya Mashariki.

Zinazojulikana kimataifa ni kwa mfano:

Viungo vya Nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii kuhusu mambo ya utamaduni bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Pasta kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.