Muungo kemia

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Muungo wa kikemia)

Muungo kemia (kwa Kiingereza: chemical bond) ni kani inayoshikiza atomu, ioni na molekuli na hivyo kuwa msingi wa kutokea kwa kampaundi.

Kani hiyo inaweza kutokana na kani umemetuamo (electrostatic force) katika muungo ionia au na muungo kovalensi ambapo atomu zinashirikiana elektroni.

Muungo wa ioni[hariri | hariri chanzo]

Muungo ionia unashikiza atomu zake, zinazopatikana kwa umbo la ioni, kutokana na tofauti ya chaji za ioni. Hutokea hasa kwenye chumvi mbalimbali yaani kampaundi za metali na simetali zinazopangwa kwa muundo wa fuwele.

Muungo wa molekuli (kovalensi)[hariri | hariri chanzo]

Muungo kovalensi wa 2x hidrojeni na 1x oksijeni kuunda molekuli ya maji; oksijeni huwa na elektroni 6 kwenye mzingo wa nje; pamoja na elektroni 2 za atomu 2 za hidrojeni inafikia namba 8, yaani kujaza nafasi zote. Vivyo hivyo atomu za hidrojeni hutumia elektroni 1-1 ya oksijeni kujaza mzingo wake.

Elementi simetali zinafanya muungo kwa kushirikiana elektroni kwenye mzingo elektroni wa nje. Atomu zinaelekea kufikia hali ambapo mzingo elektroni wa nje unajaa nafasi zote zinazowezekana. Mfano: atomu sahili ya hidrojeni ina mzingo mmoja wenye elektroni moja tu. Hii ni sababu ya kwamba atomu yake inaungana kirahisi na atomu nyingine ya hidrojeni kuwa molekuli ambapo atomu mbili za hidrojeni zinashirikiana elektroni zake na hivyo kufikia idadi ya juu inayowezekana katika mzingo wa ndani, yaani elektroni mbili. Vivyo hivyo hidrojeni inaungana kirahisi na elementi tofauti ambazo ziko tayari kupokea elektroni yake kwa kukamilisha mzingo wa nje.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Wikiquote ina mkusanyiko wa dondoo kuhusu:
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii kuhusu mambo ya kemia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Muungo kemia kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.