Mtori (shukrabenedic)

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Mtori ni chakula maarufu nchini Tanzania kinachotengenezwa kwa kutumia ndizi na nyama, lakini pia huweza kuwa na viambato vingine ndani yake (kama vile viazi, maziwa au kream)[1]. Chakula hiki asili yake ni kutoka katika eneo la mkoa wa Kilimanjaro nchini Tanzania, hasa eneo la Wilaya ya Moshi na mkoa wa Arusha[2].

Ndizi au ndizi za kijani mara nyingi huliwa katika eneo hili kama chanzo kikuu cha wanga[1]. Tangu wakati huo aina hii ya chakula imeenea katika maeneo mengine kote nchiniTanzania[3]. Katika utengenezaji wa Mtori, Kijadi fimbo maalum hutumiwa kusaga ndizi[2]. Mtori mara nyingi huliwa na wanawake wa Kimasai katika kipindi cha miezi mitatu baada ya kujifungua kwa ajili ya lishe[4]. Katika kipindi hiki cha baada ya kujifungua, wanawake hupewa hasa vyakula laini (laini) kula kama mtori[5].

Kwa sababu ni chakula chenye nguvu, kinaweza kutumiwa kama chakula kuu[6]. kinaweza kuliwa wakati wa kifungua kinywa, chakula cha mchana, au chakula cha jioni[1].

Marejeo;

  1. 1.0 1.1 1.2 Kitu Kizuri (kwa Kiingereza). Kitu Kizuri LLC. 2008. 
  2. 2.0 2.1 Riyamy, Alya Sened (2001). African Gardens: The Cuisine of Zanzibar and the East African Coast (kwa Kiingereza). Riyamy Publications. 
  3. Gall, Timothy L.; Hobby, Jeneen (2009). Worldmark Encyclopedia of Cultures and Daily Life: Africa (kwa Kiingereza). Gale. ISBN 978-1-4144-4883-1. 
  4. Horn, Corinna (2013-09-16). Maasai Cooking (kwa Kiingereza). Books on Demand. ISBN 978-3-7322-8040-7. 
  5. Seura, Suomen Antropologinen (1999). Shifting Ground and Cultured Bodies: Postcolonial Gender Relations in Africa and India (kwa Kiingereza). University Press of America. ISBN 978-0-7618-1388-0. 
  6. Webb, Lois Sinaiko (2000). Multicultural cookbook of life-cycle celebrations. Internet Archive. Phoenix, AZ : Oryx Press. ISBN 978-1-57356-290-4.