Mto Assegaai

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Ramani

Mto Assegaai umeanzia kaskazini mwa Wakkerstroom, Mpumalanga, Afrika Kusini[1], na hutiririkia kwenye bwawa Heyshope, kusini mashariki mwa Piet Retief.

Huingiapo Eswatini hufahamika kama mto Mhkondvo na hukatiza katika milima na kutengeneza korongo Mahamba. Ndani ya Eswatini mto huu hutiririka kuelekea kaskazini mashariki na hatimaye kuishia kwenye Mto Usuta.[2]

Matawimto ya mto Assegaai hujumuisha Mto Ngulane, Mto Anysspruit, Mto Boesmanspruit, na Mto Klein Assegaai.

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. Assegai River, tovuti ya za.geoview.info, iliangaliwa Oktoba 2019
  2. Ünver, Olcay, ed. (2009). "Swaziland". The United Nations World Water Development Report 3: Facing the Challenges. London: Earthscan for World Water Assessment Programme, UNESCO. p. 9. ISBN 978-1-84407-840-0. 
Makala hii kuhusu maeneo ya Afrika bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Mto Assegaai kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.