Nenda kwa yaliyomo

Monique Séka

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Monique Séka
Jina la kuzaliwaMonica Seka
Amezaliwa22 Novemba 1965 (1965-11-22) (umri 60)
Kazi yakeMwimbaji
Miaka ya kazimiaka ya 1980-hadi sasa

Monique Séka (amezaliwa 22 Novemba 1965; jina la utani la malkia wa muziki wa Afro-zouk) ni mwimbaji kutoka Ivory Coast. Kwa muziki mchanganyiko ambao anautengeneza, muziki wa Afro-zouk wa Monique Seka ni maarufu sana huko nchini kwake Ivory Coast, Afrika, Caribbean na Bahari ya Hindi.[1][2]

Maisha na muziki

[hariri | hariri chanzo]

Monique Séka alianza kuonesha shauku ya muziki tangu akiwa mtoto. Anawakilisha kizazi cha tatu cha nasaba ya muziki ya Ivory Coast. Monique ni binti wa Seka Okoi, mwimbaji maarufu wa Kivory Coast katika miaka ya 1970. Alifundishwa na baba yake kabla ya kujiunga na bendi ya RTI Orchestra. Wakati huo, alijaribu kuchanganya midundo miwili tofauti ili kuunda mtindo wa Afro Zouk, mchanganyiko ambao ulivutia wapenzi wengi wa muziki wa wakati huo.

Mnamo miaka ya 1980, muziki wa Kikaribi ulienea katika masoko ya dunia. Monique alijiingiza katika mzunguko huu na kutoa albamu yake ya kwanza, Tantie Affoué, mwaka 1985. Mnamo mwaka wa 1989, alisaini mkataba na mpigaji kinanda na mtayarishaji maarufu kutoka Cape Verde, Manu Lima, na kutoa albamu yake ya Missounwa. Mchanganyiko wake wa zouk na midundo ya Afrika ulisafiri nje ya mipaka ya bara la Afrika, na kumjengea umaarufu katika vyombo vya habari vya ndani na vya kimataifa.

Mnamo mwisho wa mwaka 1992, alikutana na Dominique Richard, mwanachama mwanzilishi wa Radio Sun, redio ya kwanza ya watu weusi wa Kikaribi iliyozinduliwa Julai 1993. Dominique akawa mtayarishaji na msimamizi wake. Wawili hawa walifunga ndoa mnamo 31 Machi 1995. Baada ya kutoa albamu kadhaa, walipata binti aitwaye Carolyn Richard, alizaliwa 9 Februari 1998.

Mnamo mwaka wa 1994, Monique alirudi kwa Manu Lima kwa ajili ya mipango ya albamu yake mpya, na kurudi nchini kwao kwa ajili ya albamu ya Okaman. Albamu zake za baadaye ni pamoja na Adéba (1997), Yélélé (1999), Anthology (1999), Miaka 15 ya Mafanikio (2003), Obligada (2005), pamoja na albamu nyingine nyingi. Mafanikio yake yamempa usaidizi kutoka kwa wasanii wengine wa muziki, ikiwa ni pamoja na Yaye Demin, ambapo walifanya wimbo pamoja na Meiway.[3][4]

  1. "La diva de la musique ivoirienne Monique Séka se confie : " J'ai peur des hommes "ses raisons | AbidjanTV.net". AbidjanTV.net (kwa American English). 2017-04-22. Iliwekwa mnamo 2017-11-24.
  2. "Marema, Singuila et Salif Keita mettent le feu au FEMUA 10 | Life Magazine". Life Magazine (kwa Kifaransa). 2017-04-29. Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2019-07-08. Iliwekwa mnamo 2017-11-24. {{cite news}}: More than one of |accessdate= na |access-date= specified (help)
  3. "Hommage à feu Okoua Séka Athanase : Monique Séka en attraction à Assuédji". Abidjan.net. Iliwekwa mnamo 2017-11-24.
  4. "Monique Séka". Music In Africa. Iliwekwa mnamo 2017-11-24.
Makala hii kuhusu mwanamuziki fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Monique Séka kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.