Monique Séka

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Monique Séka
Jina la kuzaliwaMonica Seka
Amezaliwa22 Novemba 1965 (1965-11-22) (umri 58)
Kazi yakeMwimbaji
Miaka ya kazimiaka ya 1980-hadi sasa

Monique Séka (amezaliwa 22 Novemba 1965; jina la utani la malkia wa muziki wa Afro-zouk) ni mwimbaji kutoka Ivory Coast. Kwa muziki mchanganyiko ambao anautengeneza, muziki wa Afro-zouk wa Monique Seka ni maarufu sana huko nchini kwake - Ivory Coast, Afrika, Caribbean na Bahari ya Hindi.[1][2]

Maisha na muziki[hariri | hariri chanzo]

Séka alianza kuonesha kuwa na shauku ya kupenda muziki tangu akiwa mtoto. Anawakilisha kizazi cha tatu cha ya muziki nasaba ya Ivory Coast. Monique Seka ni binti wa Seka Okoi - mwimbaji wa Kivory Coast ambaye alikuwa maarufu katika miaka ya 1970. Monique Seka alifundishwa na baba yake kabla ya kujiunga na bendi ya  RTI Orchestra. Wakati huo alikuwa anajaribu kuchanganya midundo miwili tofauti ili kuunda Afro Zouk, mchanganyiko ambao ulileta mshangao na kuwavutia wapenzi wengi wa muziki wa wakati huo huo. Katika miaka ya 1980, muziki wa Kikaribi ulivamia masoko ya dunia. Monique alijiingiza katika mzunguko huu na kuthubutu kutoa albamu yake ya kwanza iliyootwa  "Tantie Affoué" mnamo mwaka wa 1985. Katika mwaka wa 1989, alisaini mkataba na mpigaji kinanda na mtayarishaji maarufu wa kutoka Cape Verde Manu Lima na kutoa albamu yake ya "Missounwa". Hii mchanganyiko wa zouk na midundo ya Afrika alisafiri nje ya mipaka ya Afrika kwa lengo kujitangaza katika vyombo vya habari vya ndani na nje. Wakati wa mwisho wa mwaka 1992, likutana Dominique Richard, mwanachama mwanzilishi wa Radio Sun, redio ya kwanza ywa watu weusi wa Kikaribi iliyoanzishwa mwezi Julai 1993. Dominique akawa mtayarishaji na msimamizi wake.  Mnamo tarehe 31 Machi, 1995, wawili hawa wamefunga ndoa na baada ya kufanikiwa kutoa albamu kadhaa hatimaye wakapata binti aitwaye  Carolyn Richard, alizaliwa Februari 9, 1998. Mwaka wa 1994, anamwendea hewani tena  Manu Lima kwa ajili ya mipango ya albamu yake mpya na kurudi nchini kwao kwa ajili ya albamu ya "Okaman". Albamu zake za baadaye  "Adéba" mwaka 1997, "Yélélé" mwaka 1999  na nyengine kibao zilizokuja na majina mapya: "Anthology" mwaka 1999, mwaka 2003 katoa "15 Years of Success", 2005 katoa "Obligada", na nyengine nyingi tu. Mafanikio yake yamempatia kuungwa mkono na wasanii wengine wa muziki mmoja wapo ni  "Yaye Demin", walifanya ote wimbo wa Meiway.[3][4]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]