Mmenyuko wa kikemia
Mmenyuko wa kikemia, (pia utendanaji wa kikemia[1]; kwa Kiingereza: chemical reaction) ni mchakato ambao unasababisha mabadiliko ya dutu ya kikemia kuwa dutu tofauti.
Mfano mmojawapo ni moto (mmenyuko kati ya oksijeni hewani na kampaundi za kaboni).
Kimsingi katika mimenyuko hiyo elektroni za dutu zinazotendana zinahama na kuunda au kuondoa muungo kemia kati ya atomu husika. Mchakato ama unahitaji nishati au unaachana na nishati. Viini vya atomu havibadiliki isipokuwa kama elementi zinazoshiriki ni nururifu na nzito sana na hivyo si thabiti.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]
Marejeo zaidi[hariri | hariri chanzo]
- Atkins, Peter W. (2006). Physical Chemistry, 4th, Weinheim: Wiley-VCH. ISBN 978-3-527-31546-8.
- Brock, William H. (1997). Viewegs Geschichte der Chemie (in German). Braunschweig: Vieweg. ISBN 978-3-540-67033-9.
- Brückner, Reinhard (2004). Reaktionsmechanismen, 3rd (in German), München: Spektrum Akademischer Verlag. ISBN 978-3-8274-1579-0.
- Wiberg, Egon, Wiberg, Nils and Holleman, Arnold Frederick (2001). Inorganic chemistry. Academic Press. ISBN 978-0-12-352651-9.
- "Chemical Action" . Encyclopædia Britannica. 6 (11th ed.). 1911. pp. 26–33.
![]() |
Makala hii kuhusu mambo ya kemia bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Mmenyuko wa kikemia kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |