Majadiliano:Thenashara

Yaliyomo ya ukurasa hayatumiki katika lugha nyingine.
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Thenashera - mitume?[hariri chanzo]

Ni kweli ya kwamba "thenashera" inatumiwa kwa mitume 12 wa Yesu lakini katika sehemu za Biblia tu si kawaida kote. Naijua Union Version pekee lakini sina picha kuhusu matoleo yaliyo kawaida katika kanisa katoliki. (Siku zangu - ni zamani kidogo- hata wakatoliki wa Mbeya walitumia Union Version kwa sababu ilikuwa toleo la pekee lililopatikana).

Kwa maana ya kidini najua neno hili latumiwa (mara chache) kwa kundi kubwa la dhehebu la Shia (Uislamu) (linganisha: ar:شيعة اثنا عشرية na cs:Isná ašaríja) na hivyo ndivyo jinsi nilivyoikuta Zanzibar.

Tukiweka mitume 12 tungepaswa kuweka pia maimamu wa Washia sivyo? Kwa sababu hii nimeondoa orodha tena lakini sipingi ikirudishwa kama kuan sababu nzuri.

Ningependelea tuanzishe makala mpya ya 12 (namba) kwa ajili ya maana ya namba. "Thenashera" jinsi ilivyo ina maana yake maalumu inayoweza kutajwa chini ya makala ya "12 (namba)" vilevile lakini si kinyume chake. --Kipala (majadiliano) 20:55, 9 Machi 2009 (UTC)[jibu]

Napenda nijue nini maana ya neno Agape, hasa linapo tumika Upendo wa Agape.

Nugu, soma hapa: Agape na safari ijayo usisahau kutia sahihi kwenye michango yako kwa kuongeza mwishoni ~~~~ itakayobadilika kuonyesha jina lako baada ya kuhifadhi. Kipala (majadiliano) 09:51, 10 Machi 2015 (UTC)[jibu]