Lango:Sayansi/Makala iliochaguliwa/1

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Darlingtonia Californica
Darlingtonia Californica

Biolojia ni elimu ya uhai na viumbehai kama vile mimea, wanyama, kuvu (kama uyoga), bakteria na virusi.

Biolojia inaangalia jinsi viumbehai vinavyoishi na jinsi vinavyohusiana kati yao na katika mazingira yao. Lugha ya kisayansi katika biolojia inatumia maneno mengi ya asili ya Kigiriki na Kilatini. Lugha nyingi zimeingiza maneno haya tu katika msamiati wao; katika lugha kadhaa wataalamu wametafsiri sehemu ya maneno haya kwa lugha zao lakini kwa ujumla sehemu kubwa na majina ya kisayansi hufuata utaratibu wa Kigiriki na Kilatini.