Lango:Sanaa/Wasifu uliochaguliwa/1

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Vasili Vereshchagin
Vasili Vereshchagin

Vasili Vasilyevich Vereshchagin (Kirusi: Василий Василиевич Верещагин 1842 - 1904) alikuwa mchoraji kutoka Urusi aliyefahamika sana kutokana picha zake za vita na mapigano.

Alikuwa mtoto wa mkulima aliyepata elimu kwenye shule ya kijeshi akandelea kuwa afisa wa jeshi la Urusi. Aliondoka jeshini akawa mwanafunzi wa uchoraji huko Sankt Peterburg akamaliza masomo yake kwenye Chuo cha Sanaa mjini Paris.

Kama afisa wa jeshi alipata nafasi ya kuongozana na jeshi la Kirusi kwenye kempeni zake katika Asia ya Kati. Aliona vita kali na mauaji mengi akaamua kuonyesha uharibifu wa vita kwa umakini kwa matumaini ya kwamba watu wangekataa vita baada ya kuona ubaya wake. Kwa hiyo alichora mara nyingi maiti, askari wajeruhiwa, uharibifu wa vijiji na mahospitali.