Kizole

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Kizole
Kizole mabawa-mekundu
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Ngeli: Aves (Ndege)
Oda: Passeriformes (Ndege kama shomoro)
Familia ya juu: Muscicapoidea (Ndege kama shore)
Familia: Sturnidae (Ndege walio na mnasaba na kwenzi)
Jenasi: Onychognathus
Hartlaub, 1849
Ngazi za chini

Spishi = 11:

Vizole ni ndege wadogo kiasi wa jenasi Onychognathus katika familia Sturnidae. Wanatokea Afrika tu isipokuwa kizole Somali na kizole Arabu ambao wanatokea nchi za kiarabu pia. Wanapenda kuwa kwa makundi. Ndege hawa wana mabawa mekundu yaonekanayo sana wakiruka anwani. Manyoya ya dume ni meusi na yale ya jike yana rangi ya kijivu cheusi. Hula wadudu na matunda hasa, lakini hula nusra kila kitu. Hulijenga tago lao juu ya kipande cha jabali kilichojitokeza nje katika mahali penye kulindwa. Kizole mabawa-mekundu hutaga mijini pia juu ya vishubaka au mahali pengine penye kulindwa. Jike huyataga mayai 2-4 buluu.

Spishi za Afrika[hariri | hariri chanzo]

Picha[hariri | hariri chanzo]