Kizamiachaza

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Kizamiachaza
Kizamiachaza wa Ulaya
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Ngeli: Aves (Ndege)
Oda: Charadriiformes (Ndege kama vitwitwi)
Familia: Haematopodidae (Ndege walio na mnasaba na vizamiachaza)
Jenasi: Haematopus
Linnaeus, 1758
Spishi: H. ater Vieillot, 1825

H. bachmani Audubon, 1838
H. chathamensis Hartert, 1927
H. finschi G.H. Martens, 1897
H. fuliginosus Gould, 1845
H. leucopodus Garnot, 1826
H. longirostris Vieillot, 1817
H. meadewaldoi Bannerman, 1913
H. moquini Bonaparte, 1856
H. ostralegus Linnaeus, 1758
H. palliatus Temminck, 1820
H. unicolor J.R. Forster, 1844

Vizamiachaza ni ndege wa jenasi Haematopus, jenasi pekee ya familia Haematopodidae. Ndege hawa ni weusi au weusi na weupe na wana domo na macho nyekundu na miguu pinki au myeupe. Huonekana pwani kwa kawaida ambapo hutafuta chakula wakiingiza domo lao kwa matope. Hula wanyamakombe, mwata, nyungunyungu na lava wa wadudu, pengine wanyama ngozi-miiba, kaa na samaki pia. Ndege wanaokula wanyamakombe wana domo lenye ncha nyembamba kama ubapa na hulitumia kulifungua kombe ikikata musuli wa mnyama. Wale wanaokula nyungunyungu wana domo kama msharasi. Hii ni kwa sababu ya uchakavu. Vizamiachaza hutaga mayai 2-4 chini ndani ya tundu ya kina kifupi.


Spishi za Afrika[hariri | hariri chanzo]

Spishi za mabara mengine[hariri | hariri chanzo]

Picha[hariri | hariri chanzo]