Kiunzi cha mifupa

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Kiunzi mifupa)
Kiunzi cha binadamu

Kiunzi cha mifupa ni jumla ya mifupa kwenye mwili wa mtu na wanyama. Mwanadamu ana kiunzi cha ndani na mifupa ni sehemu imara chini ya ngozi na nyama ya mtu na kusudi lake ni mwili ushikamane na kuwa thabiti lakini inaruhusu pia mwendo wa viungo kimoja-moja.

Muundo wa kiunzi cha mifupa

Mfumo wa kiunzi cha mifupa cha wanyama kordata ni mifupa thabiti inayounganishwa kwa gegedu. Mifupa hii inasogezwa kwa musuli zinazofungwa kwa mfupa kwa kano. Gegedu inapatikana kwa mamalia hasa kwenye viungo vya mifupa. Kuna wanyama wengine kama papa ambako kiunzi chote kimejengwa kwa gegedu.

Pamoja na kupa mwili uthabiti na kuruhusu mwendo mifupa ni pia nafasi ya kuhifadhi minerali hasa kalsi na fosfati.

Sehemu kuu ya kiunzi cha mifupa ni uti wa mgongo. Unashika mifupa yote kwa pamoja kuanzia fuvu hadi mabavu hadi mifupa ya chini inayokutana katika fupanyonga. Unakinga ndani yake pia neva kuu zinazoelekea kutoka ubongo kwenye fuvu hadi sehemu mbalimbali ya mwili.

Kiunzi cha binadamu huwa na mifupa 206. Mifupa inaunganishwa kwenye viungo kwa nyugwe inayowezesha mwili kuwa nyumbufu. Kano huunganisha mfupa na misuli ikipeleka nguvu ya misuli kwa mfupa.

Kati ya wanyama kuna pia aina zenye kiunzi cha nje au zisizo na kiunzi. Arithropodi kama wadudu huwa na kiunzi cha nje.

Sehemu za kiunzi

Makala hii kuhusu mambo ya anatomia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Kiunzi cha mifupa kama matumizi yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.