Kituo cha angani

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Kituo cha Anga)
Kituo cha angani cha MIR, mnamo 1995

Kituo cha angani (kwa Kiingereza: Space station) ni satelaiti inayozunguka Dunia kwenye njiamzingo ya kudumu ikibuniwa kubeba wanaanga. Kusudi lake ni kuwezesha wanaanga kukaa kwenye anga-nje kwa kipindi fulani na kuendesha utafiti wa kisayansi wa aina mbalimbali. Kinaweza kutembelewa na vyombo vya angani kama feri ya anga na kwa njia hiyo wanaanga wanaweza kufika au kurudi duniani na kupokea vifaa, fueli na chakula.

Tangu mwaka 2000 kuna Kituo cha Angani cha Kimataifa. Kilitanguliwa na vituo mbalimbali kama vile MIR (Urusi), Skylab (Marekani) na Tiagong (China).

Shabaha ya vituo vya angani ni kuchunguza athira ya hali pasipo mvutano kwa mwili na nafsi ya binadamu na kutumia maabara zake kwa majaribio ya kisayansi[1]. Wanaanga hukaa kwa wiki au miezi kadhaa. Mwanaanga aliyekaa kwenye kituo cha angani kwa muda mrefu zaidi alikuwa Valeriy Polyakov (siku 437 kwenye MIR)[2]. [3].

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. Space Stations. Oracle Thinkquest. Jalada kutoka ya awali juu ya 2014-02-24. Iliwekwa mnamo 20 February 2012.
  2. A History of Manned Space Missions. National Earth Science Teachers Association. Iliwekwa mnamo 4 May 2012.
  3. A history of space stations. Cable News Network (23 November 1998). Jalada kutoka ya awali juu ya 2013-01-19. Iliwekwa mnamo 25 May 2012.
Makala hii kuhusu mambo ya teknolojia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu mada hiyo kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.