Kasuku

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Kasuku
Kasuku Mkia-mwekundu
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Nusufaila: Vertebrata (Wanyama wenye uti wa mgongo)
Ngeli: Aves (Ndege)
Oda: Psittaciformes (Ndege kama kasuku)
Ngazi za chini

Familia 4; familia 2 na jenasi 8 katika Afrika:

Kasuku ni ndege wa oda Psittaciformes. Spishi za jenasi nyingine zinaitwa kwao au cherero. Kasuku wengine ni wakubwa, wengine wadogo. Wengi wana rangi kali. Wana mkia mrefu na miguu yao ina vidole viwili vikabilivyo mbele na viwili vikabilivyo nyuma. Domo lao lina nguvu sana na mataya yamepindika kwa pande za kuelekea kama koleo. Kasuku wanatokea kanda zote za tropiki za dunia. Hula mbegu, kokwa, matunda na macho ya maua, pengine wadudu na wanyama wadogo pia. Spishi za “lories” na “lorikeets” hula mbochi na matunda mororo. Kasuku takriban wote hutaga mayai yao tunduni kwa mti.

Spishi za Afrika[hariri | hariri chanzo]

Jenasi za mabara mengine[hariri | hariri chanzo]

Picha[hariri | hariri chanzo]