Joan Maloof

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Joan Maloof mnamo 2022

Joan Maloof (alizaliwa 1956/1957) ni mwanaharakati na mwandishi wa mazingira kutoka Marekani.[1] Alianzisha Old-Growth Forest Network (Mtandao wa Misitu ya Ukuaji wa Kale) mnamo 2012.[2]

Maloof alilelewa huko Delaware. Baba yake alikuwa mhandisi wa kemikali.[1] Ni mwandishi wa vitabu vitano. Cha kwanza, Teaching the Trees , kilichapishwa mnamo 2005, na cha pili, Among the Ancients, mnamo 2011.[1][3] Mnamo 2017, alichapisha The Living Forest na mpiga picha Robert Llewellyn.[4]

Ni profesa wa heshima (baada ya kustaafu) katika Chuo Kikuu cha Salisbury.[5][6]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu mtu huyo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Joan Maloof kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.