Nenda kwa yaliyomo

El Ninyo

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Athari za El Ninyo juu ya hali ya hewa.
Athari za La Ninya juu ya hali ya hewa.

El Ninyo (pia: El Nino, kutoka Kihispania El Niño, tamka "ninyo") ni tukio la hali ya hewa linalotokea kwenye nusutufe ya kusini ya dunia kila baada ya miaka kadhaa. Dalili za El Ninyo ni kuongezeka kwa mvua kushinda hali ya kawaida.

El Ninyo ni tukio la eneo la Bahari Pasifiki lakini athari zake zinaweza kugusa maeneo mengine; pia Afrika ya Mashariki iliwahi kuona mvua mkali kutokana na El Ninyo.

Jina El Ninyo kwa Kihispania linamaanisha "mtoto" kwa maana ya "mtoto Yesu" kwa sababu hutokea wakati wa Krismasi yaani sherehe ya kuzaliwa kwa Yesu. Jina lilibuniwa na wavuvi wa Peru walioona uhaba wa samaki baharini wakati wa tukio hilo.

Jina kamili la kitaalamu ni "El Ninyo-mbembeo wa kusini" (El Niño-Southern Oscillation (ENSO)).

El Ninyo hutokea kama halijoto ya maji kwenye uso wa bahari ya Pasifiki inapanda juu ya kiwango cha kawaida. Mkondo wa maji ya vuguvugu unatokea kila mwaka mnamo wakati wa Krismasi kwenye pwani ya Ekuador na Peru na kwa kawaida hudumu wiki chache. Lakini kila baada ya miaka 2-5 unaendelea kwa miezi kadhaa.

Kuwepo kwa maji ya vuguvugu kunaongeza mvuke hewani ambayo ni msingi wa kuongezeka kwa mvua katika maeneo fulani pamoja na ukame usio kawaida katika sehemu nyingine. Australia na Asia ya Kusini Magharibi huwezi kuona ukame lakini jangwa la Peru kuona mvua nyingi. Katika Afrika ya Mashariki yote miwili inaweza kutokea ama ukame au mvua nyingi. Mabadiliko hayo yanaathiri kilimo.

Makala hii kuhusu mambo ya sayansi bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu El Ninyo kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.