Dschinghis Khan

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Dschinghis Khan [1] (kwa chi nyingine inafahamika kama[2] Genghis Khan) [3] [4] ni bendi ya pop ya disco ya Ujerumani barani Ulaya. Iliundwa huko Munich mnamo 1979 kushiriki kwenye Mashindano ya Wimbo wa Eurovision na wimbo wao "Dschinghis Khan".

Mnamo mwaka 2018, kumekuwa na vikundi viwili: vilivyoongozwa na washiriki wa asili Henriette Strobel na Edina Pop, na kundi la sasa zaidi lililoongozwa na mwanachama wa asili Wolfgang Heichel na Stefan Track, ambao walichukua nafasi ya marehemu Louis Potgieter katika tamasha la kuungana tena mwaka 2005 .

Kazi[hariri | hariri chanzo]

Kuanzia: 1970- 1980s

Bendi iliundwa na kusimamiwa na mtayarishaji wa Ujerumani Ralph Siegel. Wimbo wao wa asili uliojulikana uliandikwa na kutayarishwa na Ralph Siegel na maneno ya Bernd Meinunger na alikuja katika nafasi ya nne kwenye Mashindano ya Wimbo wa Eurovision mnamo mwaka 1979 huko Jerusalem.

Wajerumani wa asili katika kikundi hicho walikuwa Karl-Heinz "Steve", na Wolfgang Heichel, ambaye alimleta mkewe mzaliwa wa Uholanzi Henriette (née Strobel) naye kwenye tamasha hilo. Louis Hendrik Potgieter (Genghis Khan) alikuwa ni mzawa wa Afrika ya Kusini. Edina Pop (Marika Késmárky) alikuwa Mhungari ambaye alikuwa ameanza kazi yake ya uimbaji huko Ujerumani Magharibi mnamo 1969. Leslie Mándoki, ambaye pia ni Mhungari, alikuwa ameondoka Hungary mnamo mwaka 1975.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]