Nenda kwa yaliyomo

Diogo Jota

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Diogo Jota
Diogo Jota
Jina kamili Diogo José Teixeira da Silva
Tarehe ya kuzaliwa (1996-12-04)4 Desemba 1996
Mahali pa kuzaliwa Porto, Ureno
Tarehe ya kifo 3 Julai 2025 (umri 28)
Mahali pa kifo Cernadilla, Uhispania
Urefu 1.78 m
Uzito
Nchi Ureno
Taarifa za Michezo
Michezo Mpira wa miguu
Nafasi / Aina ya tukio Mshambuliaji, Winga
Timu / Klabu ya mwisho Liverpool Football Club
Kocha (wa mwisho) Jürgen Klopp
Mafanikio makubwa Mshindi wa UEFA Nations League (2019, 2025)
Tuzo / Mashindano
Mashindano UEFA Nations League, Euro
Medali / Tuzo 🥇 UEFA Nations League 2019 (Ureno)
🥇 UEFA Nations League 2025 (Ujerumani)
Taarifa nyingine
Saini

Diogo José Teixeira da Silva (anajulikana kama Diogo Jota; 4 Desemba 1996 - 3 Julai 2025) alikuwa mchezaji wa soka wa Ureno ambaye mara ya mwisho alicheza katika klabu iliyopo katika ligi kuu ya Uingereza iitwayo Liverpool Football Club.[1]

Kazi ya klabu

[hariri | hariri chanzo]

Atlético Madrid

[hariri | hariri chanzo]

Mnamo 14 Machi 2016, Jota alikubali mkataba wa miaka mitano akiwa na klabu ya Atletico Madrid.[2] Mnamo 26 Agosti alirudi katika nchi yake na kujiunga na klabu ya FC Porto kwa mkopo wa mwaka mmoja. Mnamo 1 Oktoba alifunga goli la kwanza katika ushindi wa 4-0 dhidi ya C.D. Nacional.

Wolverhampton Wanderers

[hariri | hariri chanzo]

Mnamo 25 Julai 2017, Jota alihamia katika klabu iiliyopo nchini Uingereza iitwayo Wolverhampton Wanderers kwa mkopo wa muda mrefu.Alifunga goli lake la kwanza 15 Agosti, ushindi wa magoli 3-2 dhidi ya Hull City.

Mnamo 30 Januari 2018, ilitangazwa kuwa katika mpango wa kudumu katika klabu ya Wolverhampton Wanderer. Alifunga magoli 17 bora katika mwaka wake wa kwanza.

Alifariki dunia pamoja na mdogo wake kwa ajali ya gari.

  1. David Segar (2024-01-24). "Is Ruthless Diogo Jota Liverpool's Most Clinical Forward?". Opta Analyst (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2025-07-11.
  2. Alberto R. Barbero y G. Lafora, Madrid (2016-03-14). "El Atlético ficha a Diogo Jota". Marca.com (kwa Kihispania). Iliwekwa mnamo 2025-07-11.