Chuo Kikuu cha Zürich

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Chuo Kikuu cha Zürich

Chuo Kikuu cha Zürich ni chuo kikuu kikubwa kabisa katika nchi ya Uswisi, kipatikanacho katika jiji la Zurich, NA kilicho na zaidi ya wanafunzi 26000.

Kilianzishwa mwaka 1883 kutokana na vyuo vidogo vilivyokuwapo vya elimu ya dini, sheria , utabibu na kitivo kipya cha falsafa kilichoanzishwa.

Kwa sasa chuo hiki kina jumla ya vitivo saba ambavyo ni falsafa, utabibu wa binadamu, hisabati, sheria, sayansi asilia, elimu ya dini na utabibu wanyama.

Chuo kinatoa masomo mengi na kozi nyingi ukilinganisha na taasisi zingine za elimu ya juu nchini Uswisi.