Chimbuko la mwanadamu

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Chimbuko la mwanadamu ni suala linalochochea utafiti mwingi wa akiolojia, ili kuelewa wapi walitokea watu wa kwanza. \

Suala hilo ni muhimu kwa fani mbalimbali, dini ikiwemo.

Kwa sasa wataalamu karibu wote wanakubaliana kwamba chimbuko la mwanadamu lilikuwa barani Afrika, lakini wanaleta ushahidi tofauti ili kupendekeza Afrika Mashariki, Kusini mwa Afrika, Afrika Magharibi au Afrika Kaskazini.

Sehemu ya bonde la Ufa lijulikanalo kama bonde la Oltupai lililoko ndani ya Hifadhi ya Serengeti nchini Tanzania ndiko kulikogunduliwa masalia ya kale kuliko yote yanayojulikana hivi sasa kati ya viumbehai wanaokaribiana na binadamu.

Ushahidi wa kisayansi unaotokana na nyayo za zamadamu zilizogunduliwa eneo la Laetoli lililoko kusini kidogo mwa Oltupai umeongeza hoja kuwa Tanzania au nchi jirani ni chimbuko la binadamu.