Buabua

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Buabua
Buabua domo-kubwa
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Ngeli: Aves (Ndege)
Oda: Charadriiformes (Ndege kama vitwitwi)
Familia: Sternidae (Ndege walio na mnasaba na buabua)
Jenasi: Anous Stephens, 1826

Chlidonias Rafinesque, 1822
Gelochelidon Brehm, 1830
Gygis Wagler, 1832
Hydroprogne Kaup, 1829
Larosterna Blyth, 1852
Onychoprion Wagler, 1832
Phaetusa Wagler, 1832
Procelsterna Lafresnaye, 1842
Sterna Linnaeus, 1758
Sternula Gould, 1843
Thalasseus Boie, 1822

Buabua ni ndege wa familia Sternidae. Watu wengi huita ndege hawa shakwe kama spishi za familia Laridae. Wengine hutumia jina buabua kwa spishi za jenasi Anous na Chlidonias. Spishi za jenasi Gygis ni nyeupe kabisa, zile za Sterna ni nyeupe na zina utosi weusi; spishi nyingi zina madoa meusi kwa mabawa pia. Spishi za Chlidonias zina zaidi ya rangi nyeusi, hata kwa mwili wao, na spishi za Anous zina rangi nyeupe chache tu. Buabua wana domo refu kadiri lenye ncha kali. Wanaweza kuogelea na wana ngozi kati ya vidole vyao.

Kama shakwe, buabua huhusiswha na pwani, lakini spishi nyingi wanatokea mbali na bahari, kwa kawaida karibu na maji. Huwakamata samaki wakipiga mbizi, lakini spishi za Chlidonias huwakamata wadudu pia kutoka juu ya maji baridi. Hulitengeneza tago lao chini, mara nyingi kisiwani.

Spishi za Afrika[hariri | hariri chanzo]

Spishi za mabara mengine[hariri | hariri chanzo]

Picha[hariri | hariri chanzo]