Alice Alldredge

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Alice Louise Alldredge (alizaliwa Denver, Colorado, Marekani, 1949) ni mwanabiolojia wa bahari wa Marekani ambaye anachunguza tufaha lya bahari, mzunguko wa kaboni, vijidudu na planktoni katika ekolojia ya bahari.

Alice Alldrege amafanya utafiti katika bahari wazi,katika maabara yake katika huko Chuo Kikuu cha California, Santa Barbara, pamoja na ushirikiano na Mtandao wa Utafiti wa Muda Mrefu wa Ekolojia (LTER) katika eneo la Utafiti wa Muda Mrefu wa Ekolojia ya Miamba ya Matumbawe ya Mo'orea (MCR LTER) huko Mo'orea, Polynesia ya Kifaransa.

Wasifu[hariri | hariri chanzo]

Alice Alldredge alihitimu elimu ya sekondari Merrit Hutton huko Thornton, Colorado, na kumaliza shahada ya kwanza ya biolojia katika Chuo cha Carleton mnamo 1971.

Baba yake alikuwa na msukumo kwa hamu ya mwanae katika sayansi na mama yake alikuwa mfano wa kuigwa pia. Aliendelea na masomo yake hadi kupata PhD mnamo 1975 kutoka Chuo Kikuu cha California, Davis. Kati ya 1975 na 1976, alisoma katika Taasisi ya Australia ya Sayansi ya Baharini kama Mshirika wa Udaktari wa NATO.