Solomoni wa Bretagne

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mt. Solomoni III katika mchoro wa ukutani.

Solomoni III wa Bretagne (kwa Kibretoni: Salaün; alifariki Bretagne, leo nchini Ufaransa, 25 Juni 874) alikuwa mfalme wa Bretagne kuanzia mwaka 857.

Ili kufidia uuaji wa ndugu yake alioufanya kanisani ili kujitwalia madaraka alijitahidi sana kuanzisha majimbo na monasteri na kudumisha haki.

Hatimaye alipofushwa na kuuawa na maadui wake kanisani vilevile[1].

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu[2].

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe ya kifodini chake[3].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. https://www.santiebeati.it/dettaglio/92252
  2. "Salomon". DEON.pl (kwa Kipolandi). Iliwekwa mnamo 2021-06-13. 
  3. Martyrologium Romanum
Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.