Nii Quaynor

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Nii Narku Quaynor, ni mwanasayansi na mhandisi wa Ghana ambaye amekuwa na jukumu muhimu katika kuanzishwa na kuendeleza Mtandao kote Afrika .

Wasifu[hariri | hariri chanzo]

Quaynor alihitimu sayansi ya uhandisi kutoka Chuo cha Dartmouth mnamo 1972 na akapokea shahada ya Uhandisi kutoka Shule ya Uhandisi ya Thayer mnamo 1973. Kisha alisoma Sayansi ya Kompyuta, na kupata MS kutoka Chuo Kikuu cha Jimbo la New York huko Stony Brook mnamo 1974 na shahada ya Uzamivu kutoka taasisi hiyo hiyo mnamo 1977. Alisoma Shule ya Ufundi ya Sekondari ya Kinbu, Chuo cha Adisadel na Shule ya Achimota nchini Ghana .

Yeye ni mmoja wa wanachama waanzilishi wa Idara ya Sayansi ya Kompyuta Chuo Kikuu cha Cape Coast nchini Ghana, na kwasasa ni uprofesa huko. [1] Yeye pia ni mjumbe wa Baraza la Chuo Kikuu cha Ghana.

Mnamo 2000, alikua mkurugenzi wa ICANN katika eneo la Afrika.

Quaynor aliporejea Ghana kutoka Marekani mwanzoni mwa miaka ya 1990 alianzisha mtandao ya kwanza barani Afrika na alihusika katika kuanzisha baadhi ya mashirika muhimu, likiwemo African Network Operators Group (AfNOG). [2]

Quaynor anahudumu kama Kamishna wa Tume ya Kimataifa ya Utawala wa Mtandao.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. "Prof Nii Quaynor biography". Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2007-12-23. Iliwekwa mnamo 2007-12-18. 
  2. ""Dr. Nii Quaynor Receives 2007 Jonathan B. Postel Service Award".". Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2008-02-10. Iliwekwa mnamo 2008-01-12. 
Makala hii kuhusu mtu huyo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Nii Quaynor kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.