Majengo (Mbeya mjini)
| Kata ya Majengo | |
| Mahali pa Majengo katika Tanzania | |
| Anwani ya kijiografia: 8°53′24″S 33°25′48″E / 8.89°S 33.43°E | |
| Nchi | Tanzania |
|---|---|
| Mkoa | Mbeya |
| Wilaya | Mbeya Mjini |
| Idadi ya wakazi | |
| - Mji | 3,475 |
Kwa maana mengine ya jina hili angalia hapa
Majengo ni jina la kata ya Wilaya ya Mbeya Mjini katika Mkoa wa Mbeya, Tanzania. Kwa mujibu wa sensa iliyofanyika mwaka wa 2002, kata ina wakazi wapatao 3,475 waishio humo. [1]
Majengo ni kati ya sehemu za kale kabisa za mji wa Mbeya. Mbeya ilipoanzishwa na Waingereza mnamo mwaka 1927 ilipangwa kufuatana na kawaida ya miji wa kikoloni ya Afrika ya Mashariki kuwa na sehemu tatu:
- Uzunguni kama sehemu ya nyumba za Wazungu na kando lake ofisi za serikali (District Officer, polisi, mahakama) *Uhindini kama mtaa wa biashara iliyokuwa hasa mkononi mwa wafanyabiashara wenye asili ya Uhindi ya Kiingereza na
- Majengo kama sehemu kwa wafanyakazi Waafrika na familia zao.
Marejeo [hariri]
- ↑ 2002 Population and Housing Census General Report (en). Government of Tanzania. Rudishwa juu ya 2008-08-18.
| Makala hii kuhusu maeneo ya Mkoa wa Mbeya bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Majengo (Mbeya mjini) kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
| Kata za Wilaya ya Mbeya Mjini - Tanzania | ||
|---|---|---|
|
Foresti • Ghana • Iduda • Iganjo • Iganzo • Igawilo • Ilemi • Ilomba • Isanga • Isyesye • Itagano • Itende • Itezi • Itiji • Iwambi • Iyela • Iyunga • Iziwa • Kalobe • Maanga • Mabatini • Maendeleo • Majengo • Mbalizi Road • Mwakibete • Mwansekwa • Mwansanga • Nonde • Nsalaga • Nsoho • Nzovwe • Ruanda (Mbeya) • Sinde • Sisimba • Tembela • Uyole |
||