Limpopo (mto)

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mto wa Limpopo
Mto wa Limpopo mwaka 2000
Chanzo Milima ya Witwatersrand katika Gauteng nchini Afrika Kusini
Mdomo Bahari ya Hindi
Nchi Afrika Kusini, Botswana, Zimbabwe na Msumbiji.
Urefu 1,600 km au 1,800km
Kimo cha chanzo takriban 1,700 m
Tawimito Krokodil, Marico, Olifant
Mkondo 800 m³/s
Eneo la beseni km² 414,524

Limpopo ni mto wa kusini mwa Afrika unaoishia katika Bahari Hindi.

Chanzo kipo katika milima ya Witwatersrand, kati ya Pretoria na Johannesburg, nchini Afrika Kusini. Sehemu ya kwanza inaitwa "Krokodil" (Kiafrikaans kwa mamba). Baada ya kupokea mto wa Marico jina linabadilika na kuwa Limpopo. Hapo unapita mwendo wa upinde mkubwa ukielekea kwanza kaskazini-magharibi halafu mashariki hadi Bahari Hindi. unafuata mpaka kati ya Afrika Kusini na Botswana, halafu mpaka wa Afrika Kusini na Zimbabwe.

Tawimto mkubwa ni mto Olifants (Limpopo) (Kiafrikaans kwa tembo) unaojiunga na Limpopo katika Msumbiji km 200 kabla ya mdomo wake. Mto unafikia Bahari Hindi kwenye mji wa Xai-Xai (Msumbiji).

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu maeneo ya Afrika bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Limpopo (mto) kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.