Karani tamba

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Karani tamba
Karani tamba
Karani tamba
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Nusufaila: Vertebrata (Wanyama wenye uti wa mgongo)
Ngeli: Aves (Ndege)
Oda: Accipitriformes (Ndege kama vipanga)
Familia: Sagittariidae (Karani tamba)
Jenasi: Sagittarius
Spishi: S. serpentarius
(J. F. Miller, 1779)

Karani tamba (Sagittarius serpentarius) ni ndege mkubwa wa ardhini ambaye huwinda wanyama wengine. Yeye hupatikana katika maeneo mengi Barani Afrika, mara nyingi katika maeneo tambarare na katika maeneo ya nyika ya Afrika.

Ingawa anaainishwa katika oda ya Accipitriformes, ambayo ni ya ndege wengi wawindaji wanaoonekana mchana kama vile mwewe, shakivale, tai na kipondya, karani tamba amepewa familia yake ya kipekee iitwayo Sagittariidae.

Ndege huyu huonekana katika nembo ya nchi za Sudan na Afrika Kusini.

Sifa[hariri | hariri chanzo]

katika Bustani ya Wanyama ya San Diego, Marekani
Karani tamba anatembea alikofungiwa katika bustani ya wanyama ya Ueno Zoo

Karani tamba anafahamika wazi kutokana na mwili wake unaofanana wa tai, na miguu yake inayofanana ya korongo, inayomfanya aonekana mrefu zaidi hata kufikia urefu wa mita 1.3 (futi 4). Ndege huyu mwenye urefu wa sentimita 140 (futi 4.5) ana kichwa kinachofanana cha tai na mdomo uliojipinda kwenda chini, lakini ana mabawa ya mviringo.

Uzani wake wa wastani ni kilo 3.3 (paundi 7.3) na upana wa mabawa ni mita 2 (futi 6.6).

Kwa umbali au anapopaa angani, yeye hufanana korongo bali si ndege wa kuwinda. Mkia una manyoya mawili marefu yanayoonekana kuwa marefu kuliko miguu yake anapopaa, na pia ana mkusanyiko wa manyoya yanayotengeneza umbo kama la nundu. Manyoya ya kupaa ya karani tamba na mapaja yake ni meusi, huku manyoya mengine yakiwa rangi ya kijivu na mengine yakiwa meupe.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu ndege fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Karani tamba kama uainishaji wake wa kibiolojia, maisha au uenezi wake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.