Hesse
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Hesse (Kijerumani:Hessen) ni moja ya majimbo 16 ya kujitawala ya Ujerumani lenye wakazi milioni 6,1 kwenye eneo la 21 114 km². Mji mkuu ni Wiesbaden. Waziri mkuu ni Roland Koch (CDU).
[hariri] Jiografia
Hesse imepakana na majimbo ya Ujerumani ya Rhine Kaskazini - Westfalia, Saksonia ya chini, Thuringia, Rhine-Palatino, Baden-Württemberg na Bavaria.
Miji mikubwa ni pamoja na Frankfurt, Wiesbaden, Kassel, Darmstadt, Offenbach, Marburg, Fulda, Gießen, Wetzlar, Hanau na Bad Homburg.
Rhine, Lahn na Main ni mito muhimu zaidi.

