Chromi

Kutoka Wikipedia


Chromi
Fuwele ya Chromi
Fuwele ya Chromi
Jina la Elementi Chromi
Alama Cr
Namba atomia 24
Mfululizo safu Metali
Uzani atomia 51.9961
Valensi 2, 8, 13, 1
Densiti 7.14 g/cm³
Kiwango cha kuyeyuka 2180 K (1907 °C)
Kiwango cha kuchemka 2944 K (2671 °C)
Asilimia za ganda la dunia 1,9 · 10−2 %
Hali maada mango

Chromi ni elementi na metali yenye namba atomia 24 na alama Cr katika mfumo radidia wa elementi. Ni metali ngumu na bambaikaji yenye rangi kifedha-kijivu inayopatikana katika madini na kampaundi mbalimbali.

Hutumiwa sana katika aloi za feleji na kuongeza ugumu.

Madini za chromi huchimbwa hasa Afrika Kusini (50 % ya mahitaji yote ya dunia), halafu Kazakhstan (15,2 %), Uhindi (12,1 %), Zimbabwe (3,7 %) na Ufini (3 %).

Image:WikiLettreMini.png Makala hiyo kuhusu "Chromi" bado ni mbegu. Unaweza kusaidia kuikuza kwa kubofya kitufe kilichoandikwa "hariri".

Ikiwepo makala kuhusu Chromi kwa lugha nyingine, unaweza kuitafsiri kwa Kiswahili.

Vifaa binafsi