Canterbury

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Jiji la Canterbury
Skyline ya Jiji la Canterbury
Jiji la Canterbury is located in England
Jiji la Canterbury
Jiji la Canterbury
Mahali pa mji wa Canterbury katika Uingereza
Coordinates: 51°16′30″N 1°5′13″E / Expression error: Unexpected < operator Expression error: Unexpected < operator / Expression error: Unexpected < operator; Expression error: Unexpected < operator
Nchi Uingereza
Mkoa South East
Wilaya Kent
Idadi ya wakazi
 - Mji 43,432
Website: www.canterbury.co.uk

Canterbury ni mji wa mkoa wa Kent, kusini mwa Uingereza, si mbali na London. Una wakazi 42.259 (2001).

[hariri] Historia

Ulianza kukaliwa karne nyingi K.K. na kuitwa Cantuaria. Baada ya kuvamiwa na Warumi chini ya Julius Kaisari mwaka 55 K.K. ulifanywa Forum commerciale (yaani mahali pa biashara).

Kuanzia mwaka 560 ukawa mji mkuu wa ufalme wa Kijerumani wa Kent, na mwaka 597 Augustino wa Canterbury akitokea Roma akaanzisha huko dayosisi ya kwanza ya Kilatini katika kisiwa cha Britania. Kwa ubatizo wa mfalme, uinjilishaji ulipiga hatua kubwa.

Tangu hapo, mji huo ukawa na umuhimu hasa upande wa Ukristo, kwa sababu dayosisi hiyo ilizaa taratibu nyingine zote za kisiwa hicho.

Kwa msingi huo, Askofu mkuu wa Canterbury akawa mkuu wa Maaskofu wote wa Uingereza, halafu wa Waanglikana wote duniani.

[hariri] Picha