Alfabeti
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Alfabeti: Kilatini , Kikirili , Kilatini pamoja na Kikirili , Kigiriki , Kigeorgia na Kiarmenia
Abjadi: Kiarabu , Kiarabu pamoja na Kilatini , Kiebrania pamoja na Kiarabu
Abugida: Kihindi ya Kaskazini , Kihindi ya Kusini , Kiethiopia , Kithaana Mwandishi wa kizalendo wa Kanada ,
Alama kwa neno lote na alama za silabi: Alama za neno lote , Mchanganyiko wa alama za maneno na silabi , Mchanganyiko alfabeti na silabi Mchanganyiko alfabeti na silabi
Alfabeti ni kiasi cha alama zinazotumiwa kuandika sauti za lugha fulani. Alama hizi hupatikana kama orodha kwa ufuatano uliokubaliwa, kwa mfano "a,b,c,d,e".
Jina la "alfabeti" hutokana na mwandiko wa Kigiriki ambamo herufi mbili za kwanza ni α "alfa" na β "beta".
Alfabeti huonyesha sauti si maneno kamili - hii ni tofauti na mwandiko kama Kichina mwenye alama kwa ajili ya neno lote.
[hariri] Mifano ya Alfabeti
Alfabeti inayotumiwa zaidi kimataifa ni alfabeti ya Kilatini. Lakini kuna alfabeti kadhaa zinazojulikana kimataifa kama vile:
- Alfabeti ya Kilatini (au "alfabeti ya Kirumi")
- Alfabeti ya Kigiriki hutumiwa kwa lugha ya Kigiriki.
- Alfabeti ya Kiarabu hutumiwa kwa Kiarabu, Farsi na Urdu.
- Alfabeti ya Kiebrania hutumiwa kwa Kiebrania na Kiyidish
- Alfabeti ya Kikyrili hutumiwa kwa lugha za Kislavoni kama Kirusi, Kibulgaria, Kiserbia na pia lugha za Asia ya Kati.
Mengine ni alfabeti kama vile Kikopti, Kigeorgia, Kiarmenia na vingine.
[hariri] Abugida
Aina ya pekee za alfabeti ni miandiko ya "abugida". Hii inamaanisha namna ya kuandika ambako hakuna alama za pekee kwa ajili ya vokali. Kila alama ya konsonanti ina namna mbalimbali ya kuonekana kwa kuongeza alama ndogo inayoonyesha ni vokali ipi inayofuata. mifano yake ni
| Makala hiyo kuhusu "Alfabeti" bado ni mbegu. Unaweza kusaidia kuikuza kwa kubofya kitufe kilichoandikwa "hariri". Ikiwepo makala kuhusu Alfabeti kwa lugha nyingine, unaweza kuitafsiri kwa Kiswahili. |

