Albert Szent-Györgyi
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Albert Szent-Györgyi (16 Septemba, 1893 – 22 Oktoba, 1986) alikuwa mwanakemia kutoka nchi ya Hungaria. Pamoja na nchi yake ya kuzaliwa alifanya kazi katika nchi mbalimbali kama Uholanzi, Ujerumani, Uingereza na Marekani. Alichunguza mambo mengi ya biokemia, na anajulikana hasa kwa utafiti wake wa vitamini C. Mwaka wa 1937 alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Tiba.

