Abimeleki

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Abimeleki alivyochorwa na Guillaume Rouillé katika Promptuarii Iconum Insigniorum.
Mchoro wa Gustave Doré, Kifo cha Abimeleki.

Abimeleki (kwa Kiebrania אֲבִימָלֶךְ, ’Ǎḇîmeleḵ[1]) mwana wa Gideoni [2] alikuwa mfalme wa Shekemu kwa muda mfupi wakati wa Waamuzi wa Biblia[3].

Kadiri ya Waamuzi 9:1-5 alipata ufalme kwa kuua ndugu zake wote 70, isipokuwa Yothamu aliyenusurika. Huyo alitoa hotuba yenye mfano dhidi ya Abimeleki na watu wa Shekemu waliomuunga mkono (Waamuzi 9:7-15).

Baada ya vita mbalimbali, alijeruhiwa vibaya na mwanamke aliyemrushia kutoka juu jiwe kubwa kichwani. Hapo aliagiza msaidizi wake ammalize kwa upanga.

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. His name can best be interpreted as "my father is king"
  2. Waamuzi 8:31
  3. chapter nine

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu mtu wa Biblia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Abimeleki kama habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.