Walatini

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Walatini ni kabila la kale linalodhaniwa kuvamia sehemu ya Italia ya kati (mkoa ambao leo unaitwa Lazio na makao makuu yake ni Roma) katika milenia ya 2 KK.

Polepole Roma, mji wao mkuu, uliteka maeneo mengi ya Ulaya kusini, Ulaya magharibi, Afrika kaskazini na Mashariki ya kati, hata kuunda dola kubwa lililoendelea hadi mwaka 476 magharibi na 1453 mashariki.

Kutokana na uenezi huo, utamaduni na lugha vyao vimeathiri sana dunia yote hata leo. Mfano mmojawapo ni alfabeti yao, ambayo inatumika kwa lugha nyingi duniani kote.