Uyakinifu

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Uyakinifu ni msimamo wa kifalsafa unaodai vyote ni mata tu, kwa kukanusha hasa uwepo wa roho za aina yoyote.

Hivyo mambo yote, yakiwemo ya nafsi ya binadamu, yanadhaniwa kuweza kujulikana kwa kuzingatia mata, hasa kwa njia ya sayansi.

Kwa msingi huo, uyakinifu unapinga dini, pengine kwa kuidhulumu hata kwa kutumia vyombo vya dola na kuua waumini milioni na milioni.

Ndivyo ilivyowahi kutokea na inaendelea kutokea hasa chini ya serikali zinazofuata siasa ya Ukomunisti, ambao ulijidai kuwa uyakinifu wa kisayansi.

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu: