Usindikaji

Vitu mbalimbali kutoka baharini vilivyosindikwa.
Usindikaji ni mchakato au kitendo cha kuweka vitu kwa namna malumu ili vikae kwa muda mrefu bila kuharibika.
Kuna vitu vingi vinavyoweza kusindikwa, kwa mfano: nyama, samaki, maziwa, matunda ya aina mbalimbali kama vile zabibu, maembe, machungwa na kadhalika.
Vitu hivyo hutumika katika kutengenezea bidhaa mbalimbali kama vile juisi za matunda, nyama za viwandani (za vikopo) n.k.