Unyakuzi wa Fadak

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Unyakuzi wa Fadak (kwa Kiarabu: حادثة فدك) ni tukio katika historia ya Uislamu ambamo Abu Bakr b. Abi Quhafa alinyakua Fadak kutoka kwa Fatima al-Zahra, baada ya kufariki Mtume Muhammad.

Kijiji cha Fedak kilimikiwa na mtume wakati wa makubaliano yake na Wayahudi katika vita ya khaybar. Mtume alihamisha umiliki wake wa Fadak kwa Fatima, lakini baada ya kufariki Mtume, ilinyakuliwa na makhalifa na ikakabidhiwa kwa makhalifa waliofuata wa Bani Umayya na Bani Abbas. Hata hivyo, Umar b. 'Abd al-'Aziz khalifa wa Bani Umayya na al-Ma'mun khalifa wa Abbas, walirudisha Fadak au mapato yake kwa kizazi cha Fatima.

Mtazamo wa Washia[hariri | hariri chanzo]

Kulingana na Imani ya shia Ithnashariyya, Abu Bakr ndiye aliyeimilikisha Fadak kwa khalifa ambaye alikua nbi yeye kwa kigezo cha kuizingatia/kuirejea hadith kutoka kwa Mtume —inayodaiwa kupitishwa na Abu Bakr pekee— ikisema ya kamba Mitume hawaachi chochote, lakini Fatima akajibu kwamba Mtume alimpa Fadak kabla ya kufariki kwake. akiwaomba Imam Ali na Umm Ayman kama mashahidi wake. Kwa mujibu wa vyanzo vya Shi'a na baadhi ya wanachuoni wa Kisunni, Mtume alimpa Fatima Fadak baada ya kuteremshwa Aya ya Dhawi l-Qurba ambamo Mtume aliamrishwa kutoa Dhawi l. -Qurba haki yao.

Kwa mujibu wa ripoti, Abu Bakr alishawishika na, hivyo, akathibitisha umiliki wa Fatima kupitia karatasi, lakini Umar b. al-Khattab alichukua karatasi kutoka kwa Fatima na kuirarua. Ripoti nyingine inaashiria kwamba Abu Bakr hakuwakubali mashahidi. Bibi Fatma alipogundua kwamba juhudi zake zote hazikuzaa matunda, alienda kwenye Msikiti wa Mtume na kutoa khutba. Katika khutba hii, inayojulikana kama Khutba ya al-Fadakiyya, alizungumza juu ya unyakuzi wa ukhalifa, akinukuu matamshi ya Abu Bakr mwenyewe (kulingana na ambayo Mitume hawaachi chochote) ni kinyume na aya za Qur'ani. Aliahirisha mzozo wake na Abu Bakr kwenye mahakama ya Mwenyezi Mungu katika Siku ya Kiyama na akawauliza masahaba juu ya ukimya wao juu ya dhulma kama hiyo.

Historia ya Fadak[hariri | hariri chanzo]

Fadak kilikuwa kijiji chenye rutuba karibu na Khaybar huko Hijaz, kilomita 160 kutoka Madina. Wayahudi waliishi huko na kwa sababu ya eneo lake la kimkakati, walikuwa wamejenga majumba yao kulizunguka. Baada ya Mtume kuliteka eneo la Khaybar na ngome zao wakati wa vita vya Khaybar, Mayahudi wakazi wa kasri na mashamba walituma baadhi ya wawakilishi kwa Mtume na wakaridhia kujisalimisha na kufanya suluhu na wakakubali kutoa nusu ya mashamba kwa Mtume. Mtume na wakati wowote akitaka, wanaiacha Fadak; hivyo, Mtume aliipata Fadak bila ya vita.

Inasemekana kwamba Fadak ilikuwa na mashamba mengi, bustani na mitende. Kuhusu thamani ya mitende katika Fadak, Ibn Abi al-Hadid (mwanachuoni wa Kisunni) alinukuu kutoka kwa mmoja wa watu wakubwa wa Shi'a, "mitende ya Fadak ilikuwa mingi kama mitende ya Kufa leo; na ilikuwa na mitende mikubwa."

Umiliki wa Mtume wa Fadak[hariri | hariri chanzo]

Wanachuoni wa Hadithi na waandishi wa wasifu wanakubali kwamba Fadak ilikuwa ni miongoni mwa milki safi za Mtume; kwa sababu, haikupatikana kamwe kwa vita. Kwa mujibu wa aya ya 6 na 7 za Qur'an 59, mali zilizopatikana bila vita zinaitwa fay' na Mtume alikuwa na haki ya kumpa yeyote amtakaye.

Qur'an 17:26 na kutoa Fadak kwa Fatimah[hariri | hariri chanzo]

Wafasiri wote wa Kishi'a na kundi la wanazuoni wa Hadithi wa Kisuni waliripoti kwamba ilipoteremka Aya "Wape jamaa haki yao,..." Mtume alimpa Fatima zawadi ya Fadak. Miongoni mwa wanazuoni wa Kisunni, Jalal al-Din al-Suyuti katika maelezo ya al-Durr al-manthur, al-Muttaqi al-Hindi katika Kanz al-'ummal, Tha'labi katika al-Kashf wa al-bayan, al-Hakim al-Hasakani katika Shawahid al-tanzil, Qunduzi katika Yanabi' al-mawadda na wengine wengi walisambaza ripoti hii. Maamun, Khalifa wa Bani Abbas, aliamuru kurudisha Fadak kwa watoto wa Fatimah, alikiri kwamba ilikuwa ni zawadi ya Mtume na akataja kujitolea kwake wakati wa Mtume, kwa uwazi na kukubaliwa.

Unyang'anyi[hariri | hariri chanzo]

Hadi alipofariki Mtume, Fadak ilikuwa inamilikiwa na Fatima na baadhi ya watu walifanya kazi hapo kama mawakala na wafanyakazi. Baada ya tukio la Saqifah, Abu Bakr alipofikia ukhalifa, alitangaza kwamba Fadak haikuwa mali ya mtu yeyote na akaichukua kwa ajili ya ukhalifa wake. Umiliki wa Fadak haukurudishwa kwa familia ya Mtume wakati wa ukhalifa wa Umar wala Uthman.

Mbali na Fadak, khalifa wa kwanza anadaiwa kunyakua bustani saba (al-Hawa'it al-Sab'a) kutoka kwa Fatima pia. Inasemekana kwamba bustani hizo zilimilikiwa na Mukhayriq, Myahudi aliyesilimu na akataka bustani zake apewe Mtume iwapo atauawa vitani. Aliuawa kishahidi katika Vita vya Uhud na Mtume alitoa bustani hizi saba pamoja na Fadak kwa binti yake, Fatima al-Zahra.

Ombi la Fatima[hariri | hariri chanzo]

Baada ya kutwaliwa kwa Fadak, Bibi Fatima alikwenda kwa Abu Bakr na kuzungumza naye kuhusu kurudisha umiliki wa Fadak. Kuhusu maudhui ya mazungumzo haya – ambayo yamepokewa katika vyanzo vya kihistoria na hadith zenye tofauti ndogo ndogo – imetajwa kwamba Bibi Fatima alipoomba kurudishiwa umiliki wa Fadak, Abu Bakr alisema kwamba, “Nilisikia kutoka kwa Mtume kwamba mali yake itolewe kwa Waislamu baada ya kufariki kwake na yeye hataacha mirathi yoyote.” Fatima akajibu kwamba, “baba yangu alinizawadia mali hii”-kwa hivyo si urithi. Abu Bakr alimuuliza Bibi Fatima ushahidi wa jambo hilo. Kwa mujibu wa baadhi ya vyanzo, Ali na Ummu Ayman walitoa ushahidi na kwa mujibu wa baadhi ya vyanzo vingine, Ummu Ayman na mmoja wa watumwa walioachwa huru wa Mtume walitoa ushahidi. Kwa mujibu wa baadhi ya vyanzo vingine, Imam Ali, Ummu Ayman, Imam al-Hasan na Imam al-Husayn walitoa ushahidi. Hatimaye, Abu Bakr alikubali na kuandika amri, ili kwamba mtu yeyote asiingilie Fadak. Wakati Fatima alipotoka nje ya mkutano, Umar b. al-Khattab alimwona, akaichukua amri hiyo na kuichana. Kwa mujibu wa baadhi ya vyanzo vya Kisunni, Abu Bakr hakuwakubali mashahidi wa Fatima na akawataka wanaume wawili watoe ushahidi.

Mwanachuoni wa Kisunni, Ibn Abi al-Hadid alisema, "Nilimuuliza Ibn Fariqi, mwalimu wa Baghdad, ikiwa Fatima alikuwa sahihi. Ibn Fariqi akasema, 'Ndiyo.' Nikauliza, 'basi, kwa nini Abu Bakr hakumpa Fadak?' Akasema, ‘kama angefanya hivyo, basi, Fatma angedai ukhalifa wa mumewe siku nyingine, na Abu Bakr asingeweza kukataa neno lake, kwa sababu amekubali neno lake kuhusu Fadak bila ya mashahidi.” Ibn Abi al-Hadid anaendelea: ingawa, Ibn Faraqi alisema haya kwa mzaha, lakini alikuwa sahihi."

Ingawa vyanzo vya kihistoria vimesimulia juu ya mauaji ya Muhsin katika tukio la kuishambulia nyumba ya Fatima, al-Ikhtisas anayehusishwa na al-Shaykh al-Mufid, aliitaja katika tukio la pingamizi la kunyang'anywa Fadak na akaandika kwamba. katika tukio hilo, baada ya Umar kuomba amri ya Abu Bakr, Fatima hakumpa na Umar alimpiga teke akiwa na mimba ya Muhsin na kwa teke hilo, Muhsin aliuawa. Kisha, Umar akampiga kofi Fatima usoni, akaichukua amri na kuipasua.

Ombi la Imam Ali[hariri | hariri chanzo]

Imepokewa kwamba baada ya kutekwa Fadak, Imam Ali alikwenda kwenye msikiti wa Mtume. Wakati Wahajiri na Wasaidizi walikuwepo, yeye alimpinga Abu Bakr kwa kunyang'anywa kile ambacho Mtume alimpa Fatima. Abu Bakr alimwomba shahidi wa haki ili ashuhudie kwamba Fadak inamilikiwa na Fatima. Imam Ali alitoa hoja kwamba ikiwa kitu kiko mkononi mwa mtu na mtu mwingine anadai umiliki wake, mtu anayedai ndiye anayepaswa kuleta ushahidi au mashahidi; kwa hivyo, kwa vile Fadak ilikuwa tayari mikononi mwa Fatima haitaji shahidi yeyote.

Imam Ali aliendelea kwa kusoma Aya ya al-Tathir na Abu Bakr akakiri kwamba Aya iliteremka kuhusu yeye na familia yake. Kisha akauliza: "ikiwa mashahidi wawili wangemshuhudia kwamba Fatima alizini, ungefanya nini?" Abu Bakr akasema: “Ningemfanyia hadd”. Imam akajibu: “Basi ungependelea ushahidi wa watu kuliko wa Mungu, na ungekuwa kafiri basi”. Wakati huu, watu walilia na kutawanyika. Inasemekana kwamba Imam Ali alimwandikia barua Abu Bakr vile vile na akamtishia kuhusu unyakuzi wa ukhalifa na Fadak.

Hoja ya Abu Bakr[hariri | hariri chanzo]

Imepokewa kwamba katika kuitikia maombi ya Fatima Abu Bakr alisema: “Nimemsikia Mtume akisema kwamba ‘sisi Mitume hatutoi chochote na kinachobaki kwetu ni sadaka.” Katika kujibu, Fatima aliashiria kwenye aya ya Qur'ani katika Khutba yake ya al-Fadakiyya, akichukulia matamshi ya Abu Bakr kuwa ni kinyume na Qur'ani. Zaidi ya hayo, pamoja na kuchukua maneno ya Abu Bakr kuwa yanapingana na Qur'ani, wanazuoni wa Kishia pia wanashikilia kwamba Hadith hiyo haikupokewa na yeyote isipokuwa Abu Bakr mwenyewe. Mwanachuoni wa Kisunni, Ibn Abi l-Hadid, naye ana mtazamo huo huo.

Imepokewa kwamba wakati Uthman b. Affan akiwa Khalifa, Aisha na Hafsa walikwenda kwake na kumtaka awape kile ambacho baba zao (Makhalifa wa kwanza na wa pili) walikuwa wakiwapa. Lakini Uthman akajibu: “Naapa kwa Mwenyezi Mungu kwamba sitawapa chochote…urithi? Je! ninyi wawili hamkushuhudia mbele ya baba zenu ... ya kwamba manabii hawakuusia kitu? Siku moja mnatoa ushuhuda kama huo na siku nyingine, mnaulizia urithi wa Mtume?

Khutba ya Al-Fadakiyya[hariri | hariri chanzo]

Baada ya maombi ya Bibi Fatima kwa Abu Bakr kutozaa matunda, yeye Fatma alikwenda kwenye msikiti wa Mtume na kutoa khutba kwa masahaba wa Mtume ili kulifafanua suala hilo na kuirudisha Fadak. Katika khutba hii, inayojulikana kama khutba ya al-Fadakiyya, Bibi Fatima alizungumza kuhusu kunyang'anywa kwa ukhalifa na akaukataa msimamo wa Abu Bakr na akauliza swali hili kwamba kwa mujibu wa sheria gani alimnyima urithi wa baba yake? Je, aya yoyote ya Qur'an ilisema hivyo? Kisha, yeye Fatmah aliliteremsha suala lake kwenye mahakama ya Mwenyezi Mungu Siku ya Hukumu na akawauliza masahaba wa Mtume kwa nini walinyamaza juu ya ukandamizaji huu. Bibi Fatima alisema waziwazi kwamba walichofanya (Abu Bakr na masahaba zake) ni kuvunja ahadi yao na mwisho wa khutba, bibi Fatma aliita fedheha ya kazi yao kuwa ni ya milele na mwisho wake ni motoni.

Kutoridhika kwa Fatmah[hariri | hariri chanzo]

Mbali na vyanzo vya Kishia, vyanzo vya Kisunni pia vimeripoti kwamba Fatima al-Zahra alikuwa amekasirishwa sana na Abu Bakr na Umar baada ya tukio la Fadak hadi kufa kwake kishahidi: "Fatima, binti ya Mtume, kuhuzunika na kumuacha Abu Bakr mpaka mwisho wa maisha yake.” Kuna Hadith zingine zenye athari sawa katika vyanzo vya Sunni. Imeripotiwa pia kwamba Abu Bakr na Umar walijaribu kukutana na Fatima ili kupata ridhaa yake kuhusu Fadak, lakini Fatima hakuwaruhusu. Kisha wakakutana naye kwa uombezi wa Imam Ali. Katika mkutano huu, Fatima aliashiria hadith kutoka kwa Mtume ambayo ni: "Kuriridhika kwa Fatima ni kuridhika kwangu, na hasira ya Fatima ni hasira yangu. Hivyo, kama mtu anampenda Fatima, ananipenda mimi, na kama mtu humridhisha Fatima, amenitosheleza, na mtu akimkasirisha, amenighadhibisha.” Mwishoni, Fatima hakuwasamehe.

Katika Ukhalifa wa Imam Ali[hariri | hariri chanzo]

Wakati Imam Ali alipoukubali ukhalifa kutokana na msisitizo wa watu, hakujaribu kuirejesha Fadak kwa wamiliki wake. Kama ilivyotajwa katika riwaya, kwa sababu wote Bibi Fatima na Abu Bakr wamefariki dunia wakati huo, Imam alikataa kurudisha Fadak. Imam aliamini kutaifisha Fadak ni kinyume cha sheria, na alimwachia Mwenyezi Mungu kuwahukumu watekaji.

Kuna baadhi ya riwaya katika vyanzo vya Hadith, ikiwa ni pamoja na kwamba Imam Ali mwenyewe alitaja katika khutba kwamba, "kama ningeamuru kwamba Fadak irudi kwa watoto wa Fatima, wallahi watu wangetawanyika kutoka pembeni yangu. Pia, imetajwa katika hadithi kutoka kwa Imam al-Sadiq, “Katika suala hili, Imam Ali alimfuata Mtume; kwani siku ya kutekwa kwa Makka, Mtume hakuirudisha nyumba iliyochukuliwa kutoka kwake hapo awali kwa ukandamizaji.

Katika barua kwa Uthman b. Hanif, Imam Ali alieleza kuhusu Fadak na hukumu yake. Aliandika, "Fadak ilikuwa mali yetu pekee, wakati baadhi ya watu walikuwa wakiihusudu na wengine hawakuihusudu. Mungu ndiye hakimu bora zaidi. Nina nini na Fadak au mambo mengine, wakati mahali pa mtu kesho ni kaburi."

Uchambuzi wa Wanachuoni wa Kishi'a[hariri | hariri chanzo]

Al-Sayyid Muhammad Baqir al-Sadr katika kitabu chake, Fadak fi l-tarikh, (Fadak katika historia) anazungumzia kuibua mada ya Fadak na Fatima kama hatua ya kisiasa inayowakilisha upinzani wa Uislamu na imani dhidi ya makafiri na wanafiki. Anaamini kwamba Fadak ni ishara ya lengo muhimu na mapinduzi kamili dhidi ya serikali ya wakati huo ambayo ilianzishwa huko Saqifah na watu watatu: Abu Bakr, Umar b. al-Khattab na Abu 'Ubayda al-Jarrah. Kama Bibi Fatima alikuwa tayari kurudisha Fadak kama urithi wake, kwa hakika angeweza kuleta idadi ya Waislamu wa Shi'a ili watoe ushahidi kwa ajili yake. Kwa mujibu wa uchambuzi uliowasilishwa na Baqir al-Sadr, Bibi Fatima alidhihirisha upinzani wake kwa serikali katika hatua sita.

  1. Kumtuma mwakilishi wake kwa Abu Bakr kumuuliza urithi wake (pamoja na Fadak na vitu vingine) na kumaanisha kwamba Fadak ilikuwa ni sehemu ya urithi wake kabla ya kusema kwamba Mtume alimpa kama zawadi;
  2. Kuhusika moja kwa moja na mazungumzo makali na Abu Bakr;
  3. Kutoa khutba katika Masjid al-Nabawi, siku kumi baada ya kufariki Mtume;
  4. Akitoa hotuba kwa wanawake wahajiri na wasaidizi alipokuwa katika kitanda chake;
  5. Mazungumzo mafupi na Abu Bakr na Umar akisema kwamba alikuwa amewakasirikia walipokuja kumfanyia usaliti;
  6. Kuweka wosia kwamba hataki wale waliomdhulumu washiriki katika mazishi na maziko yake.

Akichambua Khutba ya al-Fadakiyya, Shahidi anaandika, "Kwa hakika, hakutoa khutba yake kwa ajili ya kuchukua mitende ngano. Nyumba ambayo inatoa chakula chao pekee walicho nacho kwaajili ya kuwalisha wenye njaa,bila kujali matumbo yao, hawawezi kulilia chakula. Alitaka kuweka hai mila (sunna) na uadilifu. Aliogopa kwamba mawazo ya Enzi ya Ujinga, ambayo yalikuwa yamefichwa chini ya kifuniko cha Uislamu, yanajitokeza tena; na majivuno ya kikabila yanakuja kuwepo."

Mwandishi wa A'lam al-nisa' anasimulia kutoka kwa Ali b. Muhana' al-'Alawi kwamba Abu Bakr na Umar waliiweka Fadak mbali na Fatima kwa sababu waliogopa kwamba Ali angekuwa na nguvu na kuwapa changamoto juu ya ukhalifa.